Dinsdag, Januarie 30, 2024

NJOMBE YAUKATAA UDUMAVU ELIMU YAWAFIKIA WANAFUNZI

 


 

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka amewataka wanafunzi na wananchi wa mkoa wa Njombe kwa ujumla kubadili namna ya ulaji wa vyakula ili kuepukana na changamoto mbalimbali zinazotokana na ulaji mbaya, na ameshauri umuhimu wa kuzingatia lishe bora huku akisisitiza kwamba lishe bora ni kupata mlo kamili na sio kushiba kama ilivyozoeleka kwa jamii nyingi ikiwepo wanafunzi ambao baadaye ndio Taifa la Kesho.

 

Hayo aliyasema tarehe 17Januari 2024 alipofanya ziara katika shule ya Msingi Nazaleti iliyopo Halmashauri ya Mji Njombe alipokuwa akitoa elimu ya Lishe ikiwa ni mwendelezo wa Kampeni yenye lengo la kutoa elimu ya lishe kwa wazazi na walezi  na namna bora ya ulaji  unaozingatia afya.

 

‘’Lishe bora inaanza na namna ya ulaji kwani lishe bora sio kula na kushiba   hivyo ninyi kama taifa la kesho mnapaswa kuzingatia namna ya ulaji bora kutokana na changamoto mbalimbali za kiafya zinazotokana na ulaji mbaya  kwani kumekuwa na wazazi wenye tabia ya kupika vyakula leo chakula hicho kikaliwa na watoto wiki nzima sasa ninyi watoto leo tumewapa elimu hii ya lishe mkawe mabalozi kwa wazazi.amesema Mtaka

 

 

Mhe. Anthony Mtaka aliongeza  kuwa, watoto wanapaswa kula kwa kuzingatia afya jambo ambalo litasaidia kupunguza changamoto mbalimbali za kiafya ikiwa ni pamoja na Ukondefu na Udumavu kwa kutumia vyakula vinavyolinda mwili na kuwataka kuacha mara moja kula vyakula ambavyo vitawasababishia madhara ya kiafya kwa  baadaye.

 

Kampeni ya Lishe Mkoa wa Njombe inaendelea ikiongozwa  na Kauli mbiu isemayo, "Lishe ya Mwanao ni Mafanikio yake Njombe tunaweza". Kujaza tumbo si lishe jali unachomlisha.

 

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking