Dinsdag, Januarie 30, 2024

WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU AMWAKILISHA MHE. RAIS SAMIA KWENYE IBADA YA KUWEKWA WAKFU ASKOFU EUSEBIUS KYANDO MKOANI NJOMBE

 



Njombe

Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya sera, Bunge na Uratibu Mhe.Jenista Mhagama Tarehe 14 Januari 2024 alikuwa mgeni rasmi wakati wa kuwekwa Wakfu Mhashamu Askofu Dkt. Eusebius Kyando Askofu wa Jimbo la Njombe akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano  Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

 

Wakati akitoa salamu za serikali Mhe. Jenista Mhagama aliwaomba viogozi wa dini nchini kuendelea kulinda Amani na Mshikamano wa Taifa letu.  

 

Mhe.Mhagama alisema kuwa, tunu hizo ndizo zinazolitambulisha Taifa letu la Tanzania duniani na ulimwenguni kote.

 

"Tunu hizi zilindwe kwa kuzingatia umuhimu wake, pia Serikali inawashukuru viongozi wote wa dini kwakuendelea kuliombea Taifa, tunaomba muendelee kuliombea taifa bila kuchoka" alisema Mhe. Waziri

 

Mheshimiwa Waziri alipokelewa na kukaribishwa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mheshimiwa Anthony Mtaka, wakati akimkaribisha kiongozi huyo Mhe. Mtaka aliwaomba viongozi wa dini kwakushirikiana na serikali kwa pamoja kuunga mkono jitihada zinazofanywa kwenye sekta ya elimu hasa katika masuala ya Lishe kwa wanafunzi mashuleni kwa lengo la kutokomeza udumavu na utapiamlo.

 

Viongozi mbalimbali wa serikali na viongozi wa Vyama vya kisiasa walihudhulia shughuli hiyo muhimu iliyofanyika katika viwanja vya kanisa hilo.

 

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking