Woensdag, November 20, 2019

JE WAJUA MIMBA YA MWEZI MMOJA NA MAENDELEO YAKE JIFUNZE HAPA







KWA WALE AMBAO WATAHITAJI KUKUTANA  LAKINI PIA USHAURI NA MAMBO MENGINE WASILIANA NAMI  DOCTAR MWAKALINGA WASILIANA NAMI 0753121916 KWA MASHART NAAFUU.

Kwanza kabisa, Mwanamke anawezaje kushika mimba?
Wakati mwanamke ameshirikiana ngono na mwanamume, Haswaa wakati ya wiki mbili baada ya hedhi, wakati huu ambapo yai huwa limekomaa na hujiangusha au kupevuka (Ovulation), yai hili likikutana na mbegu ya mwanamume kabla lianguke kwenye tumbo ya uzazi, basi litajamiana na kuanza kupitia mchakato wa (Fertilization) kuumba mwana. Kwa wakati huu, unaweza kugundua mabadiliko mwilini mwako na umeshikwa na mshangao.

Je, nimeshika mimba?
Labda hujapata dalili za kwanza ya mimba na umekosa Hedhi(period) kwa muda fulani. Kulingana na mzunguko wako, Umetarajia kuona hedhi lakini umeikosa.
Tushazungumzia Dalili za kwanza ya mimba katika sura ya kwanza. Hebu tuvuke sasa kwa dalili hizi kimiezi.

DALILI ZA MIMBA YA MWEZI MMOJA

Kuna dalili za mimba ya mwezi mmoja isiyo kawaida sana kuzitambua. Yanayofuata ni yale ya kawaida baina ya wanawake wengi ulimwenguni.
  • Mhemko wa Hisia
  • Kujawa hewa tumboni
  • Uchungu tumboni mwa uzazi
  • Mgongo kuuma upande wa chini
  • Utoaji damu
  • Kukojoa kila wakati
  • Kufura au kujaa kwa matiti
  • Uchovu
  • Kuhisi Kutapika au kutapika
  • Ugumu wa kuenda haja Kubwa
  • Kutamani au kukataa vyakula vya aina aina
  • Kukosa Hedhi
Tilia maanani kuwa, ukiwa mja mzito mwezi wa kwanza, si lazima upitie dalili zote za mimba. Kumbuka kama mwanamke, Mungu alikupa hisia ya kujua mwili wako na ni wewe pekee unaweza kujua kama una mimba au la.
Mimba wiki ya kwanza hadi wiki ya pili?
Katika mzunguko wa hedhi, kama
mwanamke ana mzunguko wa siku ishirini na moja, yai hupitishwa wiki ya pili na hapo basi mwanamke husemekana kuwa na hedhi (period). Baada ya hiki kipindi, wiki mbili inayofuatwa mwanamke huwa na yai lililokomaa na hilo yai huachiliwa (ovulation). Yai hili lisipokutana na mbegu ya mwanamume, huachiliwa tena na huwa hedhi baada ya wiki mbili ifutayo. Hii ndio sababu wanawake waliofikisha umri wa hedhi huipata kila mwezi.
Mwanzo wa hedhi yako, mayai ishirini ambayo huitwa Ova huwa ndani ya mifuko ya follicles. Kama Hedhi yako ni ya muda wa siku ishirini na nane, hapo basi siku kumi na nne baadaye mwili wako huliangusha yai kupitia Follicles. Yai hili hupita njia ya fallopian tube ambapo litangoja kushirikiana na mbegu ya mwanamume kutengeneza uzazi.
@Mama anayesubiri
Usitie shaka kama huwezi kupata mimba mara moja baada ya kushirikaina ngono na mpenzi wako. Kulingana na umri, mwanamke ana chanzo cha kupata mwana asilimia Ishirini na tano au hadi anapofikisha umri wa  arobaini hadi hamsini. Kwa hivyo ni vizuri kujaribu mara kadhaa bila kukata tamaa.
Pia kuna wanawake wengi wanaofanya kazi ngumu ya kimwili ambao hawawezi kushika mimba mara tu wanapofanya ngono. Unapopanga wewe na mwenzio kupata mwana, ni vizuri kuwa na hali ya amani, kupunguza mawazo yanayoweza kufanya homoni ya mwili wako kukataa kushika mimba.
Kungoja wakati yai lako linapevuka ili kushirikiana ngono  ni muhimu ili chanzo chako cha kupata mwana liwe juu.
Pia kama umejaribu kumpata mwana kwa wakati wa mwaka mmoja na hujaweza kushika mimba, ni vizuri wewe na mpenziwe kushauriliana na daktari ili muweze kupata maagizo maalum kulingana na hali yenu.
Ni vizuri kujua ya kwamba sio mwanamke pekee yake anayetengeneza mwana. Wanaume pia wana sehemu kubwa zaidi katika hali hii ya kumuumba mwana. kwa hivyo ni wajibu wa wanaume na wanaweke kuwa pamoja kwa njia ya uamuzi huu.
Haya basi, hebu tuchangamkie jinsi mwana anaumbika kwa tumbo la uzazi na hali ya mwana na mamake kila wiki, inayoafikisha kila mwezi.
Ni nini kinachofanyika wiki tatu na wa nne ya mimba?
Baada ya yai limeachiliwa na likutane na mbegu ya uzazi ya kiume, mtoto huanza kuuumbika katika mchakato uitwayo fertilization.
Kuumbika kwa mtoto huwa rahisi sana haswaa kama mwanamke na mwanamume wameshirikiana ngono bila ukingaji. Sana sana siku sita na kuendelea wakati yai huachiliwa (Ovulation)
Yai lifikapo kwa mfuko wa uzazi yaani Uterus, siku tatu hadi nne baada ya kukutana na mbegu ya mwanamume, hutengeneza kiumbe kama mpira mdogo unayozunguka ndani au kuogelea ndani ya mfuko ya uzazi wa mwanamke.
Mimba huanza siku mpira huu mdogo unapojishikilia kwenye mfuko wa uzazi wa mama. Huanza tu siku sita baada mpira huu uumbike. Kumbuka ya kwamba mbegu ya mwanamke na mwanamume yanapokutana, na kuunda mpira mdogo, na huu mpira ujilaze mfukoni mwa uzazi wa mwanamke, hapo basi imesemekana kuwa una mimba.

Kupandwa au Implantation

Mimba haiji tu ki ghafla! Kuna wakati mwingi mbegu za mwanamume huingia kwenye mfuko wa mwanamke na wakati wa hedhi, mwanamke huutoa kama umwagikaji wa damu.
Kupata mimba inategemea na siku ya mwanamke anapoachilia yai na anapofanya ngono na mwanamume na mbegu ya mwanamume ikutane njiani, hapo basi kuna chanzo kubwa ya mtoto kuumbika.
Unapogundua una mimba, kuna baina ya mabadiliko, kimwili na mawazoni. Kila wakati hisa zako hubadilika. Unaweza kuhisi furaha na huzuni au kushtuka kila wakati. Kubali mwili wako na mafikira yako yawe na amani. Usifikirie u pekee yako duniani. Mimba ni baraka na watoto ni baraka. kwa sababu homoni kama vile progesterone na estrogen imeongezeka mwilini hisia mbali mbali hufuatia na kumfanya mwanamke kugeuza hali yake ya kawaida. Jilinde vema na chambua jinsi unavyoweza kujipa moyo wakati wa huu.
 “kupendana, kuzaana”
Wakati mwingine, Kuna baina ya wanawake waliosema ya kuwa wanapokuwa na mimba, hisia za kufanya ngono hubadilika. Kuna wale ambazo hisia hizi huongezeka na kuna wale hisia zao hupungua. Haya yote ni kawaida na usitie shaka.
Pia kuna wale wanawake waliosema kuwa wana ndoto za hofu au za hakika. kwa sababu homoni yako mwilini imeongezeka kufanya kazi, akili yako huwa katika hali ya kuwaza kila wakati. Kwa hivyo unapolala ni kawaid kuota ndoto za aina nyingi ambazo huwa za hofu.

Mwana wako anafanana na amekuwa kiasi gani?

Kwa wakati huu, mwana wako ni mdogo zaidi. Kimo chake kimelinganishwa na ule wa mbegu ya poppy. Amegawanyika katika vipande viwili viitwavyo  Epiblast na Hypoblast. Katika chupa cha  mama, ufuko wa kumlinda mwana huyu na kumfunika na kumlisha vema pia imenza kuundika. Mama anaweza kuhisi machungu ya aina aina wakati huu. machungu haya yanaweza kulingana na yale ya hedhi.
Ni muhimu sana mwanamke anayepitia hali hii ya kwanza kumbeba mtoto kujaribu kula vyakula bora na kupumzika zaidi ili mwili wake uweze kumlaza mwana vizuri. Ufutaji wa sigara na kunywa pombe inaweza kutayarisha hali ya mimba na ni vyema kukoma.

Mwili wako

Kwa wakati huu, Mwili wako umebaki kuwa ya kawaida na hujaonyesha mabadiliko zaidi. Ingawaje, Matiti yako yameanza kuwa makubwa na nzito, tumbo yako ni ya kawaida tu. Kuna baina ya wanawake waliosema walihisi upande wa tumbo yao limeingia ndani kiasi. Kumbuka ya kuwa kila mwanamke ana utafauti wake.

SWALA NYETI!

Je ninaweza kushirikiana ngono wakati nina mimba?
Ndiyo! Wewe na mumeo mwaweza kushirikiana ngono siku yoyote kwenye kipindi hiki cha kuwa mja mzito. Wakati wa hatari ni ule unapoanza kuhisi uchungu isiyo ya kawaida na ni jambo la muhimu kuenda kujadiliana na daktari wako.

Utajuaje mimba yako ni ya miezi mingapi?

Kuna aina mbali mbali ya kujua una mimba ya miezi mingapi. Kama kawaida, unasemekana una mimba ya mwezi mmoja katika wiki tano hadi nane ya kukosa hedhi. Kumbuka unaweza kushika mimba mapema hata kabla ujue umekosa hedhi.
 “Kuzaliwa kumoja, maisha mengi”
Kuna njia ya kuafikisha mimba yako ni ya siku ngapi au ya kufanya hesabu ya mimba uliyo nayo. Kipimo hiki huitwa The African Parent Mtoto Due Date Calculator . Hapa utaweza kufanya hesabu kulingana na siku ya kwanza ya hedhi ya mwisho, kisha itakueleza una mimba ya siku ngapi na utaweza kujifungua siku gani. Kipimo hiki ni cha kukutayarisha ili usipatwe na hofu wakati unapombeba mwana.
Ni vizuri kujadiliana na daktari wako ili ujue kwa hakika una mimba ya miezi au wiki ngapi.
Upenyo wa haraka ya mimba ya mwezi mmoja
  • Hakikisha una mimba kwa kuchukua Pregnancy test au kujadiliana na daktari wako kwa kupata uhakika sana sana ukiwa umefanya ngono bila kujikinga na pia ukiwa umekosa hedhi.
  • Usiogope kumwuliza daktari wako maswali kama jinsi unavyo stahili kujichunga. Tafuta marafiki watakaokusaidia kupitisha muda wakati unapogundua una mimba.
  • Nena na mume wako na pamoja mjadiliane vile mtamlinda mwana.
  • Jaribu Kukula vyakula vya kukupea nguvu ukiweka akilini , mtoto wako pia anahitaji vyakula halisi ili awe na afya njema. Jaribu haswaa kufanya mazoezi rahisi kama kutembea kila siku, Kunywa maji mengi na fanya mapumziko kila wakati unahisi Uchovu.
  • Kumbuka, wakati huu hisia zako huwa umechanganyikiwa. Unaweza kuhisi furaha ama kukasirika kwa haraka sana. Pia unaweza kujipata unalia sana kuliko kawaida. Tafuta njia rahisi ya kukumbana na hisia hizi.
Tafadhali Sahihi hapa chini ili uagizwe njia tofauti ya kukumbana na hali ya mimba!

mubashara blog +255753121916

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking