Vrydag, Junie 03, 2022

Habari kubwa katika Jarida letu la leo Juni 03, 2022

 

Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Andrea Tsere anaendelea kuwaasa baadhi ya watu watakao dhubutu kukwamisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022.

Kauli hiyo anaitoa kila mahala anapo endelea na ziara yake ya Kuhamasisha na kuelimisha watanzania wote waliopo ndani ya Wilaya ya Ludewa huku akiwaeleza umuhimu wa Sensa ya kwa maendeleo ya taifa letu.

Aidha Mhe. Andrea Tsere alisesema "zoezi la Sensa ya Watu na Makazi kwa mwaka huu ni muhimu kwenye taifa letu, kwani kila mmoja wetu akihesabiwa serikali itajua namna ya kuhudumia wananchi wake haswa wakati wa kuandaa bajeti ukilinganisha na idadi ya Watu wake"

Kwa kuto hesabiwa mmoja utaifanya serikali ipate takwimu tofauti hivyo watu wangu kwanu wananchi wote tarehe 23/08/2022 kila mmoja anawajibu wa Kuhesabiwa asiwepo hata mmoja wa kukwepa jambo muhimu la kitaifa.


Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking