Dinsdag, Januarie 30, 2018

ZAO LA PARETO LAPEWA KIPAUMBELE LUDEWA, SOKO LIKO WAZI NDANI NA NJE YA TANZANIA


Bw,Godfrey Mbeyela Meneja wa PARETO Mkoa wa Njombe akifafanua Ubora Wa PARETO Mbele wa Baraza la madiwani Ludewa.
Bei za PARETO kwa kilo Kulingana na Ubora wake
 Na Maiko Luoga Ludewa,
Wananchi wilayani Ludewa katika Mkoa wa Njombe wameshauriwa Kulima mazao yakibiashara Ikiwemo PARETO,KOROSHO, KAHAWA NK, yenye soko la Uhakika ndani na nje ya Tanzania ili kuweza kujikwamua Kiuchumi kutokana na Mazao mengi wanayolima Wakulima Wilayani Humo Ikiwemo mahindi Kukosa Soko Huku wakulima wakiishia Kukaa na mazao yao Ndani ya nyumba Bila kupata Faida.

Ushauri huo ulitolewa na Meneja wa Zao la PARETO Mkoa wa Njombe Bw, Godfrey Mbeyela wakati akifafanua Faida za Zao hilo katika Mkutano wa Baraza la Madiwani Kwa Robo ya Pili ya Mwaka 2017 / 2018 kwakipindi cha Kuanzia Mwezi October hadi December 2017 Mkutano uliofanyika January 27 Mwaka huu 2018 Katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa.

Meneja huyo Wa PARETO Mkoa wa Njombe aliwaomba Madiwani wote katika Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa kufikisha Ujumbe kwa wananchi katika Maeneo yao ili waweze Kulima kwa wingi Zao hilo la PARETO ambalo linaelezwa kuwa na Faida kubwa zaidi kwa Mkulima Kwakuwa PARETO Inavunwa mara kwa mara iwapo Shambani na Mkulima atauza Mazao yake kisha Kulipwa pesa yake kulingana na Mzigo Aliouza.

Akieleza Bei za Zao La PARETO Mbele ya Madiwani wa Halmashaurui ya Wilaya ya Ludewa Meneja wa Zao hilo Bw, Mbeyela Alisema kuwa kwa Msimu wa Mwaka 2017/2018 Pareto Imekuwa ikiuzwa Kuanzia Tsh, 3300 Hadi 2300 Kwa kilo Moja ya Zao hilo la Patreto huku akiwahakikishia wananchi wa Ludewa kuwa Kampuni inayojishuhgulisha na Zao hilo ndani na Nje ya Tanzania ijulikanayo kwa Jina la PYRETHRUM COMPANY OF TANZANIA LIMITED (PCT) Imejenga Kiwanda katika Eneo la Mafinga Mkoani Iringa Kwaajili ya Kununua PARETO Kwa wakulima watakao zalisha zao hilo.

Hatahivyo Kampuni ya PYRETHRUM COMPANY OF TANZANIA LIMITED (PCT) yenye Soko la PARETO ndani na Nje ya Tanzania Inatoa Miche Bure kwa wakulima wa zao hilo ambao wanahitaji Kulima zao hilo.

Katika Hatua Nyingine Meneja wa PARETO Mkoa wa Njombe  Bw, Godfrey Mbeyela ameweka Bayana Taratibu na Ushauri wa Kuuza PARETO Kiwandani kuwa ni pamoja na Wakulima kuuza PARETO yao moja kwa moja Kiwandani ili kuboresha zaidi mapato yao na Kuongeza kuwa Wakulima wanashauriwa Kujiunga katika Vikundi kuanzia watano na kuendelea pamoja na Kupata kibali au kitambulisho kutoka kwa Uongozi wa Kijiji wanapotoka, juu ya nia yao ya Kuuza Pareto moja kwa Moja Kiwandani Wakiwa na Muhtasari wa Kuanzishwa kwa kikundi chao na Kibali cha Kijiji kisha watafika Kiwandani na Kupata Mkataba Tayari kwakuuza Pareto yao.

Bw, Mbeyela Aliongeza kuwa Wakulima Baada ya Kupewa Mkataba wataelekezwa namna ya Kupata Leseni Kutoka Bodi ya Pareto Tanzania inayowaruhusu kufanya Biashara ya PARETO kisha kijiji kinashauriwa Kutunza Orodha ya Vikundi vyake vyote na nakala itawasilishwa Kiwandani.

Nchini Tanzania Zao la PARETO Linaelezwa kustawi kwa wingi katika Mikoa wa Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania katika Mikoa ya Njombe, Mbeya na Iringa na Kiasi kidogo katika kanda ya Kaskazini Mkoa wa Arusha Pia Kampuni ya PYRETHRUM COMPANY OF TANZANIA LIMITED (PCT) Inamsaidia Mkulima Bora wa Pareto Kujua namna ya kuandaa Shamba la kuzalisha Zao hilo kuwa ni Pamoja na Mkulima Kuchagua eneo lenye Rutuba ya Kutosha, Kusafisha Shamba na Kuondoa magugu yote Shambani, Pamoja na Kulima vizuri shamba la PARETO.

Baadhi ya Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe akiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mh, Edward Haule pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya Ya Ludewa Bw, Ng'wilabizu Ndatwa Ludigija, Madiwani pamoja na Watumishi wa Halmasahuri ya Wilaya ya Ludewa Wameipongeza kampuni hiyo ya  PYRETHRUM COMPANY OF TANZANIA LIMITED (PCT) Kwakuamua kulifufua zao la PARETO Katika wilaya ya Ludewa kwakuwa wananchi waliamua kuacha kuzalisha zao hilo kutokana na Ukosefu wa soko hivyo kwasasa Viongozi hao wameuahidi Uongozi wa kampuni hiyo kuwa watawaelimisha wananchi ili waweze kuzalisha zao hilo kwa wingi zaidi.

chrispiny kalinga

Tumia mchanganyiko wa papai na asali kuondoa madoa usoni


KUMEKUWA na sababu mbalimbali zinazofanya watu kutokuwa na ngozi zisizokubalika.Mbali na hali ya hewa pia matumizi ya pombe na sigara hata matumizi ya cream kali ambazo zimekuwa zikitumiwa na watu

Faida 10 za kutumia Mafuta ya Nazi


1. Mafuta ya nazi kwa afya ya Moyo:
Mafuta ya nazi yana asidi mhimu sana kwa afya ya moyo iitwayo ‘lauric acid’ ambayo ina uwezo mkubwa kuuweka moyo wako katika hali ya afya na furaha kwa kuidhibiti kolesteroli/lehemu mbaya katika moyo na mwili kwa ujumla. Lauric acid huongeza uwepo wa kolesteroli nzuri mwilini ijulikanayo kwa kitaalamu kama High Density Lipoprotein (HDL) huku ikiishusha ile kolesteroli mbaya ijulikanayo pia kwa kitaalamu kama Low Density Lipoprotein (LDL) jambo ambalo ni mhimu kwa afya ya moyo kama anavyosema Lovisa Nilsson, mtaalamu wa lishe wa Lifesum.

2. Mafuta ya nazi huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula:
Hii ndiyo moja ya faida ya mafuta ya nazi niipendayo zaidi. Ndiyo mafuta ya nazi yanayo uwezo kusaidia kudhibiti uzito uliozidi kwa sababu mafuta haya ni mepesi kumeng’enywa na hayagandi kama yalivyo mafuta mengine mazito (fatty acids) jambo linalosaidia kuuondoa uzito uliozidi mwilini. Kutokana na kitendo hiki cha kuongeza uwezo wa mwili kukimeng’enya chakula, watu wanaoyatumia mafuta haya kupikia vyakula vyao kila siku kwa kawaida huwa na uzito wa kawaida. Anasema Geeta Sidhu Robb, mtaalamu wa lishe na mwanzilishi wa Nosh Detox.

Faida 10 za kutumia Mafuta ya Nazi

1. Mafuta ya nazi kwa afya ya Moyo:
Mafuta ya nazi yana asidi mhimu sana kwa afya ya moyo iitwayo ‘lauric acid’ ambayo ina uwezo mkubwa kuuweka moyo wako katika hali ya afya na furaha kwa kuidhibiti kolesteroli/lehemu mbaya katika moyo na mwili kwa ujumla. Lauric acid huongeza uwepo wa kolesteroli nzuri mwilini ijulikanayo kwa kitaalamu kama High Density Lipoprotein (HDL) huku ikiishusha ile kolesteroli mbaya ijulikanayo pia kwa kitaalamu kama Low Density Lipoprotein (LDL) jambo ambalo ni mhimu kwa afya ya moyo kama anavyosema Lovisa Nilsson, mtaalamu wa lishe wa Lifesum.

2. Mafuta ya nazi huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula:
Hii ndiyo moja ya faida ya mafuta ya nazi niipendayo zaidi. Ndiyo mafuta ya nazi yanayo uwezo kusaidia kudhibiti uzito uliozidi kwa sababu mafuta haya ni mepesi kumeng’enywa na hayagandi kama yalivyo mafuta mengine mazito (fatty acids) jambo linalosaidia kuuondoa uzito uliozidi mwilini. Kutokana na kitendo hiki cha kuongeza uwezo wa mwili kukimeng’enya chakula, watu wanaoyatumia mafuta haya kupikia vyakula vyao kila siku kwa kawaida huwa na uzito wa kawaida. Anasema Geeta Sidhu Robb, mtaalamu wa lishe na mwanzilishi wa Nosh Detox.

Zijue mbinu Za kujitibu chunusi Bila Kutumia Na Gharama Kubwa


Chunusi ni ugonjwa wa ngozi ambao hujitokeza kama viuvimbe au vipele vidogo vidogo hasa sehemu za uso, kifuani na hata mgongoni. Vipele hivi hutokea wakati vishimo vya kupitisha jasho katika ngozi vinapozibwa kwa mafuta au seli za ngozi zilizokufa au wadudu yaani bakteria.

Aina 10 ya Wanawake Wanaopendwa na Wanaume


WENYE MSIMAMO
Wanawake daraja la kwanza wanaopendwa zaidi na wanaume ni wale wenye msimamo, uelewa mkubwa wa mambo na maamuzi sahihi, wako makini kwenye matendo yao na siku zote hufanya vitu kwa ajili ya kupata mafanikio.

Zijue sababu zinazopelekea wapenzi wengi kuchokana Mapema



Hivi uliwahi kujiuliza hivi ni kwanini baadhi ya mahusiano ya kimapenzi hufa mapema, kama si kufa basi kushuka kwa mahusiano hayo? Moja kati ya sababu ambayo husababaisha kufa kwa mahusiano ni ile tabia ya kuchokana mapema katika mahusiano na moja kati ya sababu kubwa ambayo hupelekea kuchokana mapema ni:

Zijue sifa za mpenzi asiyekupenda kwa dhati


Watu wengi hawapendi kutambua kwamba mtu anayempenda yeye hampendi, kwasababu ni maumivu makubwa sana moyoni. Unapokuwa kwenye mahusiano na mtu huyo nae inamuwia vigumu kukwambia "sikupendi" hufanya hivi katika kuzihurumia hisia zako juu yake.

Hizi ndio Faida za kunywa maji yenye ndimu asubuhi



Kunywa maji yasiyo na kitu wakati wa asubuhi huwapa tabu baadhi ya watu. Lakini maji yaliyotiwa ndimu kidogo huwa na radha nzuri zaidi.

Madhara Ya Kufanya Mapenzi Kupita Kiasi


Katika hali ya kawaida kufanya mapenzi kuna faida nyingi, lakini linapokuja suala la kuzidi kiasi tunapata matatizo ya msingi ambayo huleta madhara kwa watu wanaoendekeza sana ngono.

Madhara Ya Kufanya Mapenzi Kupita Kiasi


Katika hali ya kawaida kufanya mapenzi kuna faida nyingi, lakini linapokuja suala la kuzidi kiasi tunapata matatizo ya msingi ambayo huleta madhara kwa watu wanaoendekeza sana ngono.

Magonjwa ya kuku, Tiba na Kinga


Ugonjwa huu huathiri kuku katika umri wowote na unapoingia kwenye kundi huweza kuua idadi kubwa ya kuku hao hadi kufikia asilimia tisini. Ndege wakubwa hustahimili kidogo kuliko wale wadogo kwasababu ya usugu mwilini (body immunity) uliojengeka kwa muda mrefu zaidi.

Ugonjwa huu husababishwa na kimelea cha kirusi kiitwacho Paramyxo viridae na huenezwa kwa njia ya hewa na kugusana.


Dalili zake:

  • Kukohoa na kuhema kwa shida
  • Ute hutoka mdomoni na puani
  • Kuku walioathirika hupata kizunguzungu.
  • Kuharisha uharo wa kijani na njano
  • Kuzubaa, kusinzia na mabawa kushuka
  • Baada ya siku 2 kuku hupindisha shingo
  • Kuvimba macho
  • Kuzunguka
  • Kuku hutaga mayai hafifu.
  • 90% ya kuku huweza kufa

Tiba:
Ugonjwa huu hauna dawa.
Kinga:

Kuchanja;
Chanja kuku wako kila baada ya miezi mitatu /na mara nne kwa mwaka.
Kuna chanjo aina mbili za ugonjwa huu, nazo ni;

Lasota: Chanjo hii hutolewa katika dawa yenye umbile la kidonge kimoja kimoja ambacho kina dozi ya kuku 1000 na huwekwa kwenye maji ili kuku wanywe hiyo dawa.
Inashauriwa kuku wanaopewa dawa hii wanyimwe maji ya kunywa siku moja kabla yake
Ni  vizuri kuwapa mchanganyiko maalum wa dawa wenye mchanganyiko wa  vitamin na dawa ya kuwaongezea kuku nguvu. Dawa hii itolewe saa moja au zaidi  baada ya kuwapa chanjo ya mdondo.
Thermostable I2 NCD vaccine:
  • Huwekwa katika chupa kimoja (vial) chenye dozi 400 za kuku
  • Chanjo hii inavumilia joto ikikaa bils nje ya jokofu kwa muda mrefu zaidi.
  • Imetengenezwa katika mazingira ya nchi za joto.
Na inaweza kukaa kwa siku 14-15 ikiwa itatunzwa ipasavyo hata baada ya kutumia mara ya kwanza.
2)      Kuharisha Damu (Coccidiosis):
Ugonjwa huu husababishwa na kimelea cha protozoa cha jamii ya Eimeria (Eimeria tenela, Eimeria maxima, na Eimeria acervulina)
Kwa kawaida wadudu hawa hupenda kuishi kwenye mazingira machafu, kama vinyesi, vyakula vilivyooza na umaji maji (moist environments).
Dalili zake:
Kinyesi chake huchanganyika na damu
1)  Wakati mwingine kuku hunya damu
2)  Kuku hudhoofika sana
3)  Kuku huteremsha mabawa yake
4)  Hatimaye vifo hutokea
Kushusha mabawa.

 Kuharisha damu.


 Utumbo wenye damu
Tiba;
Ugonjwa huu hutibika kwa kutumia dawa za
(i) Kundi la suphur
Mfano: sulphonamides (ESB3) kwa siku 3-4
(ii) Amprolium
Dawa za ugonjwa huu hupatikana madukani hivyo ukipatwa na tatizo hilo fika kwenye maduka ya dawa aua muone mganga wa mifugo.
Kinga:
  • Zingatia usafi mara kwa mara
Kwakuwa ugonjwa huu huambatana na majimaji na uchafu wenye vimelea vya ugonjwa huu, ni  vizuri kuhakikisha banda la kuku linakuwa safi na kavu wakati wote.
  • Tenga kuku wagonjwa kutoka kwa walio wazima.
  • Tumia dawa ya kinga ili kuepusha uwezekano wa kuku kuambukizwa ugonjwa huu
Dawa inayopendekezwa ni zile zinzoitwa (coccidiostat.
  • Tenga kuku wadogo (vifaranga) kutoka kwenye kundi la wakubwa.
3)      Homa ya Matumbo (fowl typhoid)
Husababishwa na vimelea vya wadudu wa bakteria wa jamii ya Salmonella.
Kimelea hicho cha bacteria huitwa Salmonella gallinarum.
Dalili zake:
  • Uharo mweupe au wa kijani
  • Vifo hufikia kiasi cha 50%
  • Rangi ya minofu hugeuka kuwa ya njano
  • Viungo vya ndani kama maini , figo , bandama huvimba
  • Maini hung’aa kwenye mwanga mkali.
Tiba :Tumia dawa za antibiotiki kama vile furazolidone ili kutibu ugonjwa huu.
KINGA: Chanja kuku wako mara kwa mara .
  • Fanya usafi wa banda na vyombo vya kulishia na kunyweshea maji ipasavyo.
4)      Ugonjwa wa Mafua ya Ndege
  • Ugonjwa wa mafua ya ndege ni ugonjwa hatari sana kwa kuku na jamii nyingine za ndege.
  • Pia ugonjwa huweza kuambukizwa na kusababisha vifo kwa binadamu.
  • Ugonjwa huu husababishwa na kirusi kiitwacho Orthomyxovirus.
  • Ugonjwa huu huenezwa kwa njia ya kugusana baina ya ndege na ndege  na baina ya ndege na binadamu.
Dalili zake
Dalili za ugonjwa huu huanza kuonekana katika kipindi cha siku 3-7 baada ya kuku kuambukizwa.
Dalili hutofautiana kutokana na umri wa ndege.
Baadhi ya dalili zake nihizi zifuatazo
  • Kuku /ndege hupumua kwa shida (dyspnoea).
  • Kuzubaa.
  • Kutokwa na machozi.
  • Kukohoa na kupiga chafya.
  • Kuharisha kinyesi chenye majimaji.
  • Sehemu za kichwa zisizo na manyoya huvimba.uvimbe wenye majimaji huonekana kichwani na shingoni.
  • Sehemu ya juu kichwani hubadilika na kuwa na rangi ya bluu iliyopauka.
  • Kuku hutaga mayai yenye maganda laini.
Tiba:
Ugonjwa huu hauna tiba .
Kinga na kuzuia kuenea kwa ugonjwa huu:
  • Toa taarifa kwa mganga (daktari wa mifugo aliye karibu ukiona dalili za ugonjwa huu.
  • Tenga mabanda ya kuku wagonjwa na walio wazima.
  • Fungia kuku wako wasitembee holela.
  • Acha kununua kuku kutoka eneo linalohisiwa kuwa na ugonjwa huu.
  • Acha kusafirisha mifugo /ndege bila idhini ya daktari.
  • Zuia wageni kutembelea mabanda yako ya kuku.
  • Acha kuhamisha mbolea ya kuku kwenda shambani kutoka kwenye banda la kuku wanaoumwa ugonjwa huu.
  • Safisha mabanda na kuweka dawa chini ya usimamizi wa mtaalamu wa mifugo na kulipumzisha kwa siku 21kabla ya kuanza kufuga tena.
  • Choma moto mkali au fukia chini mbolea kutoka kwenye banda la kuku wanaoumwa ugonjwa huu.
  • Pata ushauri kutoka kwa mtaalamu wa mifugo aliye karibu nawe.
5)      Gumboro (infectious Bursal Disease)
Ugonjwa  huu husababishwa na kirusi
Dalili zake:
o   Hushambulia vifaranga
o   Uharo mweupe
o   Kuchafuka (dirting of anal area)
o   Kuvimba
o   Kiwango kikubwa cha vifo
o   Damu hutapakaa eneo la kutolea kinyesi
Kinga:
1)      Usafi
2)      lishe bora
3)      chanja vifaranga wakiwa na umri wa wiki tatu  kwa kutumia chanjo hai (live vaccine)
6)      Kifua Kikuu cha Ndege(Avian Tuberculosis-TB)
Husababishwa na kimelea aitwaye Mycobacterium avium.
Dalili zake:
o   Kukonda na Kupungua uzito
o   Vidonda  kwenye kishungi
o   Kupungua uzito/kukonda
o   Kuhara
Kinga:
Usafi:
Fanya usafi na vyombo , banda na mazingira .
7)      Magonjwa yatokanayo na Lishe (Nutritional and Metabolic Disorders)
Dalili za magonjwa haya hutegemea aina ya virutubisho vinavyokosekana mwilini
Kwa mfano:
o   Kupinda miguu (rickets) husababishwa na upungufu wa Vit.D, madini ya calcium na fosforasi.
o   Vidonda vyenye vyenye damu husababishwa na vit.K
o   Kichaa cha kuku na kusinyaa kwa misuli husababishwa na upungufu wa Vit.E
o   Magamba ya Mayai (egg shell)kuwa laini  ama umbo kuwa  bovu husababishwa na upungufu wa madini ya calcium na fosforasi.
o   Kudonoana kusababishwa kwa njia moja au nyingine na upungufu wa chakula na madini ya fosforasi na calcium
o   Kuvimba macho, upungufu wa damu huletwa na upungufu wa vit.A.
Kinga:
o   Kuwapa kuku mlo kamili
o   Kuelewa kwa kina aina za chakula kwa kila rika na aina ya kuku ; vifaranga , kuku wa mayai na wa nyama. (Poultry age and classes i.e chicks, layers and broilers)
o   Kufanya uchunguzi wa virutubisho vilivyomo katika aina ya chakula unachotumia.
8)       Minyoo (Helminthiasis)
Minyoo iko ya aina tatu kama vile minyoo kamba, minyoo bapa na minyoo ya mviringo
Dalili zake:
  • Kudumaa
  • Kuwa manyoya hafifu
  • Kupungua uzito
  • Kukonda
  • Minyoo huonekana kwenye kinyesi
Kinga /kuzuia:
USAFI:
  • Fanya usafi wa vyombo, banda na mazingira.
  • Tenga vifaranga kutoka kwa wale wakubwa.
  • Badilisha matandazo kuondoa mazalia ya minyoo.
  • Badilisha matandazo kila baada ya miezi mitatu.
Tiba:
  • Tumia dawa zinazopendekezwa na wataalamu hasa zile zinazoua minyoo ya aina zote (mfano: piperazine citrate).
  • Hakikisha kila baada ya miezi mitatu unawapa kuku wako dawa za minyoo.
9)      Kupe, Utitiri, Chawa na Viroboto
kupe laini  waitwao Argus persicus,  chawa na viroboto wanaong’ata .
Dalili zake:
  • Kujikung’uta.
  • Kupiga kelele.
  • Kiasi cha damu hupungua mwilini.
  • Utando wa ngozi ndani ya kope za macho hupauka.
  • Utando wa ngozi ya juu mwilini huwa mnene.
  • Magamba ya unga-unga hudondoka.
Kuzuia:
  • Tupa au choma masalia ya mayai yasiyoanguliwa na magamba ya mayai yaliyoanguliwa vifaranga.
Safisha banda mara kwa mara na kunyunyizia dawa; kuna dawa zinazopendekezwa na wataalamu za kunyunyizia kwenye banda la kuku. Mfano wa hizo dawa ni sevin , akheri powder n.k (Dawa hizi ni za unga).

chrispiny kalinga