'Hitmaker' wa Ngarenaro, Dogo Janja amemchana msanii Edu Boy kwa aina yake ya uimbaji ya kuwa-diss wasanii wenzake katika mashairi yake na kudai kuwa anachokifanya ni utoto mtupu na kwamba hawezi kufaidika na lolote.
Mbele ya kamera za eNEWZ Dogo Janja amesema kwamba msanii anapaswa kuimba kitu ambacho hata kizazi kijacho kikipata fursa ya kuskiliza nyimbo zao kitajifunza kitu kupitia mashairi ya msanii husika.
Dogo Janja ameendelea kusema kwamba "mpaka sasa tunasikiliza nyimbo walizoimba wasanii wa zamani kama kina Mbaraka Mwinshehe kwa kuwa waliimba nyimbo zenye maadili na zenye ujumbe kwa jamii lakini pale unapoamka na kuanza kuandika mashairi ya kumchana msanii mwenzio huwezi kuwa na historia nzuri kwenye sanaa".
Msanii huyo amedai kwamba Edu Boy ni kama mdogo wake kwenye sanaa kwa kuwa amemkuta kwenye sanaa na kusema kuandika wimbo unaowachana wasanii wezake inakuwa kama umeamka na mawazo yako alafu unaamua kuyamalizia kwa wasanii wezako kwani anachoamini ni kwamba hata ukiwachana wasanii wezako huwezi kufaidika kwa lolote.
Waziri wa kilimo Mh.Dkt.Charles Tizeba amesema serikali inakusudia kutunga sheria ya kilimo ambayo itatoa mwongozo na kanuni za kufuatwa na wadau wote wa sekta ya kilimo nchini ili kuongeza uwajibikaji zaidi na kuinua kilimo kwa shabaha ya kuondokana na kilimo cha mazoea
Mbunge na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Joseph Msukuma amemshambulia kwa maneno Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina juu ya 'operation' anazozifanya za kionevu za kupambana na uvuvi haramu kwa kumwambia aache kufanya kazi kwa mihemuko.
Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma wa CUF kwa upande wa Maalim Seif, Mbarala Maharagande amefunguka na kuweka wazi kuwa Profesa Lipumba pamoja na genge lake wamepanga njama kuwafukuza madiwani wote wa CUF Dar es Salaam.
Meneja wa mamlaka ya maji Ludewa Bw.Mwinuka Gregory akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa Pets. siku kadhaa zimepita baada ya ukaguzi huo HABARI IMEANDIKWA NA
Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Mwigulu Nchemba amelitaka jeshi la polisi kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa na kwamba taasisi hiyo ndiyo inayoshughulika na haki za watu na wasipofanya kwa uadilifu yapo madhara makubwa kwa jamii na kutoka kwa wahalifu.
Ndege mbili; moja aina ya Bombardier na nyingine kubwa Boeing 787 yenye uwezo wa kubeba abiria 262 zilizonunuliwa na serikali, zinatarajiwa kuwasili nchini Julai mwaka huu.
MAHAKAMA ya Wilaya ya Dodoma imeagiza mkazi wa mtaa wa Ng’ong’ona Manispaa ya Dodoma Tito Machibya, maarufu kama ‘Nabii Tito’ (45) kupimwa akili upya katika Taasisi ya Afya ya Akili ya Mirembe Isanga mkoani Dodoma ili kujiridhisha kama ana matatizo ya akili.