Donderdag, Maart 15, 2018

POLISI: Asiyejua kufa akachungulie kaburi

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo Jeshi la Polisi, CP Nsatu Marijan amesema hali ya usalama nchini imezidi kuimarika kwani hakuna tishio lolote la kiuhalifu linaloweza kutokea kwasababu Jeshi la Polisi limejipanga ipasavyo na halishindwi na chochote.

Mama Kanumba: Natamani Kwenda Kumuona Lulu Gerezani

Mama mzazi wa aliyekuwa msanii wa Bongo movie Marehemu Steven Kanumba, Mama Kanumba ameibuka na jipya tena huku safari hii akisema anatamani kwenda jela kumuona Lulu.

Uzinduzi wa Albamu ya Diamond Watikisa Kenya

Msanii  wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz amezindua rasmi albamu yake mpya ‘A Boy From Tandale’ jijini Nairobi na kufanya bonge la shoo akiwa na timu nzima ya WCB.

Mbali na WCB, wasanii wengine waliopada jukwaani na kutikisa katika shoo hiyo, ni msanii wa Marekani, Omario.

Albamu mpya ya Diamond imesheheni ngoma 20 kali zikiwemo alizowahi kuzitoa kipindi cha nyuma na nyingine mpya.

mubashara blog +255753121916

Afande Sele ajiunga rasmi CCM.....Rais Magufuli Ampokea

Msanii mkongwe nchini Afande sele ametangaza rasmi kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) leo mbele ya Rais Dkt. Magufuli kwa lengo ka kuunga mkono jitihada zake anazozifanya katika kupigania na kukiomba chama kimpokee kama kijana wao

Waziri Mwijage Aweka Jiwe La Msingi La Ujenzi Wa Majengo Ya Viwanda....Mavunde Awataka Wajasiriamali Dodoma Kuchangamkia Mikopo Kutoka Sido

Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mh Charles Mwijage(MB) ameweka jiwe la msingi la Ujenzi wa Majengo kwa ajili ya viwanda vidogo vidogo katika eneo la Kizota-Manispaa ya Dodoma ambapo jumla ya viwanda vidogo 45 vinatazamiwa kuanzishwa kupitia utaratibu wa Clusters “Kongani” na pia kutoa mafunzo kwa Wajasiriamali mbalimbali.

Rais Magufuli Aagiza wafanyabiashara wadogo wa Stendi Morogoro Wasibughudhiwe.....

Mwanamke aliyejitambulisha kwa jina  moja la Avintishi, leo amejitoa kimasomaso na kumueleza Rais John Magufuli kuhusu kero wanayopata wafanyabiashara ndogondogo ikiwamo kunyang’anywa bidhaa zao.

Taarifa ya Sido kwa kamati ya Bunge yakataliwa

Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira imesusia kupokea taarifa ya Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (Sido), huku ikitoa onyo kwa wateule wa Rais John Magufuli kutekeleza wajibu wao ipasavyo na kwa kasi inayohitajika.

Agizo hilo limetolewa leo Machi 15, 2018 mkoani Singida ambapo kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake, Suleiman Sadiq walipofika kutembelea viwanda kadhaa mkoani humo na mwenyeji wao alitakiwa kuwa ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage.

Akizungumzia leo, Sadiq amesema kamati ya Bunge inapotembelea anapaswa kuwapo waziri, naibu waziri au katibu mkuu, lakini “tumemkuta naibu katibu mkuu na maofisa wengine wa wizara na wale wa Sido, ambao hawakuwa wamejindaa na tumeikataa taarifa yao.”

Amesema Mwijage alipaswa kuwapo wameelezwa amekwenda Morogoro kuhudhuria ufunguzi wa kiwanda cha Sigara eneo la Kingolwira.

“Kwa sasa tupo tu tunatembea tembea hapa Singida, lakini tuseme hawa watendaji wa Rais Magufuli wanapaswa kujitambua na kutekeleza wajibu wao. Kama wameshindwa kutoa ushirikiano kwetu hata kwa kumtuma naibu waziri (Stella Manyanya) au katibu mkuu, hii Tanzania ya viwanda kweli itakuja kama hakuna ushirikiano,” alihoji Sadiq.

Sadiq ambaye ni mbunge wa Mvomero amesema, “tumsaidie Rais Magufuli na sisi katika taarifa yetu tutajua kipi cha kufanya tutakaporudi Dodoma, kwa hiyo sisi kama wabunge hatujapenda kilichotokea leo.”

mubashara blog +255753121916

Serikali ya Tanzania yaidhinisha matumizi ya dawa za asili kutibu nguvu za kiume


Dawa za asili maarufu kama 'miti shamba'Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionDawa za asili maarufu kama 'miti shamba'

Hivi karibuni nchini Tanzania kumeshamiri kwa uwepo wa matangazo mbalimbali ambayo mengine ni rasmi na mengine sio rasmi kuhusiana na dawa za asili haswa za kuongeza nguvu za kiume lakini sasa serikali ya nchi hiyo imethibitisha matumizi ya dawa tano za asili.

Na Maiko Luoga Ludewa

Wadau Wenye Viwango mbalimbali vya Elimu na Uchumi Ambao ni wazawa wa wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe wanaoishi Nje ya Ludewa wameshauriwa Kurudi wilayani Ludewa ili kusaidia Shughuli Mbalimbali za Maendeleo zinazofanywa na Wananchi katika Vijiji na Katika kata  mbalimbali wilayani Ludewa.

PICHA ZA VIONGOZI WA WILAYA YA LUDEWA PAMOJA NA WANAFUNZI


Hawa ni moja ya wanafunzi wa shule ya msingi wilaya luduwa mkoani njombe.

Mwanajeshi Anayedaiwa kuua askari mwenzake apandishwa kizimbani

Mwanajeshi MT 109795 Private Ramadhan Mlaku (28) amefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shitaka la mauaji ya askari mwenzie, MT 79512 SGT Saimon Munyama.

Uwoya Amchimba Mkwara Dogo Janja Aliposikia Anataka Kuoa Mke wa Pili

Kupitia mitandao ya kijamii kumekuwa na taarifa kuwa msanii Dogo Janja ana mpango wa kuongeza mke wa pili baada ya kufunga ndoa na muigizaji Irene Uwoya ambapo ndoa hiyo ilifungwa mwaka jana 2017 ingawa mashabiki hadi sasa hawaamini kuhusu ndoa hiyo.

Diamond: Media Zinazokataa Kupiga Nyimbo Zangu Zinapotea

Mwanamuziki wa Bongo fleva na CEO wa label ya WCB, Diamond Platnumz amefunguka na kusema kuwa chombo chochote cha habari ambacho kinaibania WCB kwa njia yoyote basi kitapotea kwani yeye ni kama maji usipokunywa utayaoga.