Vrydag, Julie 06, 2018

WANANCHI MANDA LUDEWA WAANDAMANA KWA UGOMVI WA ARDHI YA KIJIJI CHAO



Na mwandishi wetu 

Ludewa

 Huyu ni Afisa mtendaji wa kijiji cha Mmanda Wilaya ya Ludewa Mkoa wa Njombe
Prisca Jonathani Mwakakae.

Wananchi wa kijiji  cha Manga katika wilaya ya Ludewa mkoani Njombe wameandamana leo jully 6.2018
 katika ofisi za kijiji hicho wakifunga milanga ipatayo saba ya ofisi hizo kwa lengo la kutaka viongozi wa juu waende kutatua mgogolo wa aridhi ambayo inapiganiwa na Bwana Frorence Mtewele kuwa ni  mali yake na huku viongozi wa kijiji hicho wakidhibitisha kuwa ni eneo la serikali.

Katika hatua nyingine wananchi hao wamesema eneo hilo tangu zamani lilikuwa likimilikiwa na serikali ya kijiji hicho tu baada ya kupewa na mzazi wa bwana frorence mtewele ambapo kwa sasa kijiji hicho kimewekeza kwa zao miti.
Hali kadhalika Mwenyekiti wa kijiji hicho ndugu Angerusi Mgaya amezungumza na waandishi wa habari kwa kudhibitisha kuandamana kwa wananchi hao na akaongeza kwa kusema kuwa mgogoro wa eneo hili sio wa mara ya kwanza kwa kusema kuwa hata mkuu wa wilaya ya ludewa alishawahi kufika katika eneo hilo na kumaliza kuwa eneo hilo ni la serikali.
Akaongeza kwa kusema kuwa yeye kama mwenyekiti wa kijiji hicho amejalibu kuzungumza na viongozi wa kata hiyo na viongozi hao bado hawaja mpa majibu yoyote juu ya mgogoro huo.

Sambamba na hilo Afisa Mtendaji wa kijiji hicho ndugu  Prisca Jonathani Mwakakae amesema kuwa wananchi kuandamana katika eneo hilo wapo sahihi kwa kudai mali ya kijiji chao na akaongeza kwa kusema kuwa licha ya maandamano salama yeye kama kiongozi wa kijiji hicho ameamua kutoa taarifa kituo  cha polisi wailaya ya ludewa na kwa viongozi wake wa juu.
Hata hivyo ndugu Frorence Mtewele ambaye ndiye mmiliki wa eneo hilo amesema kuwa yeye eneo hilo linalo gombaniwa ni mali ya babayake tangu hapo zamani
Pia akamaliza kwa kusema kuwa kindi kilicho pita wiki kdhaa nyuma alipaelekwa mahakamani juu ya eneo hilo na mahakama ikaamuru kuwa eneo hilo ni la kwake na mahakama ikaamuru kuwa ambaye hajalika na kesi hiyo anaruhusiwa kukata rufaa.


mubashara blog +255753121916

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking