Maandag, Maart 12, 2018

Mwili wa marehemu watelekezwa nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa

Baadhi ya wananchi wa Mtaa wa Nyakabale wilayani Geita wametelekeza mwili wa marehemu nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa huu, Elias Ndarawa.

Diwani Chadema atimkia CCM, kisa biashara zake haziendi vizuri

Matukio ya Madiwani kuhama Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) yamezidi kushika kasi,  baada ya diwani wa tano wa Kata ya Olsunyai, Elirehema Nnko, kuhama chama hicho jana.

Serikali Yaanza Rasmi Mazungumzo Na Kampuni Ya Bharti Airtel Juu Ya Umiliki Wa Airtel Tanzania

Mazungumzo kati ya Kamati Maalum iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Kampuni ya Bharti Airtel inayomiliki hisa katika kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania yameanza rasmi leo tarehe 12 Machi, 2018 Jijini Dar es Salaam.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) yatahadharisha mvua kubwa mikoa 11

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya vipindi vya mvua kubwa vinavyotarajiwa kuendelea katika maeneo ya mikoa 11 nchini.

TMA imetaja mikoa itakayoathirika na mvua hizo ni Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara, Morogoro, Ruvuma, Rukwa, Mbeya, Songwe, Iringa na Njombe.

Taarifa iliyotolewa leo na mamlaka hiyo inabainisha kuwa kuanzia leo Machi 12 hadi 13 ,2018 kunatarajiwa vipindi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24.

“Hali hii inatokana na kuendelea kuimarika kwa ukanda wa mvua, wakazi wa maeneo yaliyotajwa wanatakiwa kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa na tahadhari zinazotolewa, TMA inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa mrejesho kila itakapobidi,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.


mubashara blog +255753121916

Wakili wa Abdul Nondo ( Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP)) akwama polisi

Mwanasheria Jebra Kambole na Wakili wa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo amefunguka na kusema kuwa mpaka sasa ameshindwa kuonana wala kuongea na mteja wake huyo ambaye anashikiliwa na jeshi la polisi.

Aliyemtaja Mange Kimambi, Zitto Kabwe, Tundu Lissu na wengine kuwa ni watu 10 hatari zaidi Tanzania kuburuzwa mahakamani

Mjasiriamali/Mwanahabari na Mkurugenzi wa Compass Communications, Maria Sarungi amefungua kesi ya madai katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu dhidi ya Mhariri wa Gazeti la Tanzanite na Mwanasheria Cyprian Musiba kwa kumkashifu na kuchafua jina lake kupitia mkutano wake na Waandishi wa Habari uliyofanyika tarehe 25 Februari, 2018.

Sondag, Maart 11, 2018

Furusa za kazi kwa walimu

*NAFASI ZA AJIRA KWA WALIMU: SHULE YA SEKONDARI BERTHAIDA,DAR ES SALAAM*

🔘 *WALIMU WA PHYSICS*
🔘 *WALIMU WA CHEMISTRY*
🔘 *WALIMU WA BIOLOGY*
🔘 *WALIMU WA HISTORY*
🔘 *WALIMU WA CIVICS*
🔘 *WALIMU WA KISWAHILI*
🔘 *WALIMU WA ENGLISH/LITERATURE*

ACT-Wazalendo Wameongea na Waandishi wa Habari Leo....Nini Wamekisema?, Bofya Hapa

Ngome ya vijana ya Chama cha ACT Wazalendo imewataka mawaziri wenye dhamana ya kusimamia viwanda, ajira na fedha kukaa pamoja kutafakari tatizo la ajira kwa vijana na kuweka mazingira bora ya ufanyaji wa biashara ndogondogo.

Tweet ya Kikwete yazua gumzo mtandaoni

Ujumbe wa Rais mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete katikati ya wiki hii uliteka mtandao wa kijamii wa Twitter na kusambaa kwenye Whatsapp, akionesha sehemu ya maisha yake baada ya urais.

Dkt. Kikwete ambaye alihamia Msoga mkoani Pwani kwa ajili ya mapumziko baada ya kutoka Ikulu, aliwepa picha kadhaa akiwa anakula chakula kwenye sahani na bakuli moja na wazee ambao walihudhuria msiba wa baba yake mdogo, Said Lumaliza katika kijiji cha Msigi.

“Tukila chakula na ndugu zangu msibani kwa baba yangu mdogo marehemu Said Lumaliza(1917-2018) katika kijiji cha Msigi karibu na Msoga. Hii ndiyo fahari ya maisha ya kustaafu.!” alitweet mara mbili kwa Kiswahili na Kiingereza, Machi 8.

Watumiaji wa mtandao huo ambao wengine walitoka nje ya nchi walisifu maisha ya kujishusha ya rais huyo mstaafu na kueleza kuwa ni viongozi wachache waliokuwa na cheo kama chake ambao wanaweza kurejea kwenye maisha ya aina hiyo.

“Kuna Maisha baada ya kustaafu. Itafika muda ulinzi kamili itakua ni yale uliyo wafanyia watu na ndicho nilicho jifunza hapo,” aliandika Samuel Isaya.

“Wewe ni rais wa mfano kwa Afrika pamoja na kuwa na mapungufu yako kama binadamu. Hongera sana mhe Mungu akutangulie ktk muda wote wa Maisha yako,” Zakayo Sarwatt.

“It’s very rare to see a former African president from any African country spending time with low class citizens,” aliandika Hermescash. Kwa tafsiri isiyo rasmi, “Ni mara chache sana utaona marais wa zamani Afrika kutoka nchi yoyote wakitumia muda wao na watu wa hali ya chini.”

mubashara blog +255753121916

Godbless Lema: Uhusiano Usioridhisha kati ya wabunge na viongozi wa Serikali unakwamisha shughuli za maendeleo.

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema uhusiano usioridhisha kati ya wabunge na viongozi wa Serikali unakwamisha shughuli za maendeleo.

Tafsiri sahihi ya kosa la uhaini na adhabu yake Kwa Mujibu wa Katiba ya Tanzania

Uhaini  ni  kosa  la  jinai, kwa tafsiri nyepesi ina maana kwamba ni kosa kubwa ambalo mtu analifanya dhidi ya nchi yake na mtu anyefanya kosa hili anajulikana kama msaliti, mfano wa watu wasaliti wanaojulikana duniani ni Yuda ambaye kidini alimsaliti Yesu, mwingine ni Benedict Anold huyu jamaa aliisaliti nchi yake ya Marekani dhidi ya Mbritishi, wengine ni Vidkun Quisling, na Marshall Pe’tain.

Ifahamu sheria ya maandamano Kikatiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Maandamano ya aina yoyote ni haki ya mwananchi na yanaruhusiwa kisheria lakini maandamano hayo lazima yafuate sheria na taratibu zilizobainishwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Lewo Jumapili ya March 11