Dinsdag, Januarie 30, 2024

NJOMBE YAUKATAA UDUMAVU ELIMU YAWAFIKIA WANAFUNZI

 


 

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka amewataka wanafunzi na wananchi wa mkoa wa Njombe kwa ujumla kubadili namna ya ulaji wa vyakula ili kuepukana na changamoto mbalimbali zinazotokana na ulaji mbaya, na ameshauri umuhimu wa kuzingatia lishe bora huku akisisitiza kwamba lishe bora ni kupata mlo kamili na sio kushiba kama ilivyozoeleka kwa jamii nyingi ikiwepo wanafunzi ambao baadaye ndio Taifa la Kesho.

 

Hayo aliyasema tarehe 17Januari 2024 alipofanya ziara katika shule ya Msingi Nazaleti iliyopo Halmashauri ya Mji Njombe alipokuwa akitoa elimu ya Lishe ikiwa ni mwendelezo wa Kampeni yenye lengo la kutoa elimu ya lishe kwa wazazi na walezi  na namna bora ya ulaji  unaozingatia afya.

 

‘’Lishe bora inaanza na namna ya ulaji kwani lishe bora sio kula na kushiba   hivyo ninyi kama taifa la kesho mnapaswa kuzingatia namna ya ulaji bora kutokana na changamoto mbalimbali za kiafya zinazotokana na ulaji mbaya  kwani kumekuwa na wazazi wenye tabia ya kupika vyakula leo chakula hicho kikaliwa na watoto wiki nzima sasa ninyi watoto leo tumewapa elimu hii ya lishe mkawe mabalozi kwa wazazi.amesema Mtaka

 

 

Mhe. Anthony Mtaka aliongeza  kuwa, watoto wanapaswa kula kwa kuzingatia afya jambo ambalo litasaidia kupunguza changamoto mbalimbali za kiafya ikiwa ni pamoja na Ukondefu na Udumavu kwa kutumia vyakula vinavyolinda mwili na kuwataka kuacha mara moja kula vyakula ambavyo vitawasababishia madhara ya kiafya kwa  baadaye.

 

Kampeni ya Lishe Mkoa wa Njombe inaendelea ikiongozwa  na Kauli mbiu isemayo, "Lishe ya Mwanao ni Mafanikio yake Njombe tunaweza". Kujaza tumbo si lishe jali unachomlisha.

 

WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU AMWAKILISHA MHE. RAIS SAMIA KWENYE IBADA YA KUWEKWA WAKFU ASKOFU EUSEBIUS KYANDO MKOANI NJOMBE

 



Njombe

Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya sera, Bunge na Uratibu Mhe.Jenista Mhagama Tarehe 14 Januari 2024 alikuwa mgeni rasmi wakati wa kuwekwa Wakfu Mhashamu Askofu Dkt. Eusebius Kyando Askofu wa Jimbo la Njombe akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano  Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

 

Wakati akitoa salamu za serikali Mhe. Jenista Mhagama aliwaomba viogozi wa dini nchini kuendelea kulinda Amani na Mshikamano wa Taifa letu.  

 

Mhe.Mhagama alisema kuwa, tunu hizo ndizo zinazolitambulisha Taifa letu la Tanzania duniani na ulimwenguni kote.

 

"Tunu hizi zilindwe kwa kuzingatia umuhimu wake, pia Serikali inawashukuru viongozi wote wa dini kwakuendelea kuliombea Taifa, tunaomba muendelee kuliombea taifa bila kuchoka" alisema Mhe. Waziri

 

Mheshimiwa Waziri alipokelewa na kukaribishwa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mheshimiwa Anthony Mtaka, wakati akimkaribisha kiongozi huyo Mhe. Mtaka aliwaomba viongozi wa dini kwakushirikiana na serikali kwa pamoja kuunga mkono jitihada zinazofanywa kwenye sekta ya elimu hasa katika masuala ya Lishe kwa wanafunzi mashuleni kwa lengo la kutokomeza udumavu na utapiamlo.

 

Viongozi mbalimbali wa serikali na viongozi wa Vyama vya kisiasa walihudhulia shughuli hiyo muhimu iliyofanyika katika viwanja vya kanisa hilo.

 

MKUU WA MKOA WA NJOMBE MHE. ANTHONY MTAKA AMETUMA SALAMU ZA SHUKRANI KWA MHE. RAIS SAMIA SULUHU HASSAN KWA KUTOA MBEGU YA NGANO KWA WANANCHI WA WILAYA YA MAKETE NA LUDEWA.



 Na. Chrispin Kalinga - Njombe


Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka tarehe 11 Januari 2024 aliongoza Mkutano wa Pareto na Mdau Mkuu wa PCT uliofanyika katika Ukumbi wa Madihani Villa Hotel ulipo Halmashauri ya Wilaya ya Makete.

 

Mkutano huo ulihudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Wilaya ya hiyo, Wakurugenzi wa Halmashauri na Maafisa Kilimo kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Njombe pamoja na  Wananchi wa maeneo hayo wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Makete Mhe. Juma Sweda.

 

Alipokuwa akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano huo Mhe. Mtaka alisema kuwa, Wilaya ya Makete inakwenda kukua kiuchumi kutokana na uwekezaji mkubwa unaofanywa haswa kwenye maeneo ya Kilimo cha Pareto pamoja na Kilimo cha Ngano.

 

Aidha, Mhe. Mtaka alisema kuwa, katika Halmashauri ya Wilaya ya Makete yenye kata 23, jumla ya kata 21 zinafaa kwa Kilimo cha zao la Pareto ambapo jumla ya eneo lenye ukubwa wa Hekta 2800 zinafaa kwa Kilimo cha zao la Pareto katika kata 21. 

 

Ikumbukwe kwamba zao la Pareto hapa nchini Tanzania linaumuhimu mkubwa kwa matumizi mbalimbali ikiwa ni pamoja na utengenezaji wa madawa mbalimbali ya kuua wadudu ambapo makampuni ya madawa duniani hutumia sumu ya Pareto katika kutengeneza madawa (Viuadudu), Unga wa maua ya Pareto hutumika kuhifadhi nafaka kama vile mahindi, Maharage ili yasishambuliwe na wadudu waharibifu.

 

Sambamba na hayo Mhe. Mtaka alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuutazama na kuukuza kiuchumi Mkoa wa Njombe kwenye sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na sekta ya kilimo ambapo amesema, Wilaya ya Makete ina jumla ya Maafisa Ugani Kilimo 59, ambapo kati ya hao watatu (3) wapo ngazi ya Makao Makuu ya Wilaya hiyo na Maafisa Ugani 56 wapo ngazi ya Kijiji na Kata na wote hao wamepatiwa Pikipiki kwaajili ya Utendaji kazi wa kuwahudumia wakulima. 

 

Uwepo wa Maafisa Ugani ngazi hizo unasaidia kutoa ushauri wa Kitaalam kwa wakulima ngazi ya Jamii, Watendaji wa Kata na Vijiji wanasaidia katika uhamasishaji wa Kilimo cha Pareto na Kuwezesha tija na uzalishaji kuongezeka.

 


Vrydag, Junie 03, 2022

Habari kubwa katika Jarida la Ludewa ni pamoja na Jeshi la Polisi Ludewa laendelea kutoa elimu ya unyanyasaji wa kijinsia na Wananchi





Katika Jarida letu la leo ukiondoa habari  kuu yagazeti letu Leo nimekusogezea taarifa mbalimbali kutoka ndani ya Wilaya yetu.

Na moja ya habari hizo ni pamoja na Jeshi la Polisi Wilaya Ludewa linaendelea kupaza sauti kwa kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa kuwapa elimu ya Ukatili wa kijinsia na kuwasihi watanzania wote wa Wilaya ya Ludewa kuachana na vitendo vya kikatili ambavyo hivyo hupelekea vifo.

Aidha Inspector Violeth GIdeon amepaza sauti kwa kuzifikia Tarafa zaidi 3 za Wilaya ya Ludewa kwa kuendelea kuelimisha na Kuhamasisha kutokomeza Ukatili wa kijinsia huku akibainisha kwa kuwapa uhuru wananchi wote kutoa taarifa za ukatiki wanapo ziona katika kituo chochote cha Polisi.

Wananchi hupata fursa ya kuuliza maswali na kupatiwa ufumbuzi na huku Inspector huyo akiwasihi wanawake kuacha Ukatili kwa watoto na kwawaume zao na akawasihi wanaume kutoa taarifa katika Dawati la jinsia pindi wanapo fanyiwa ukatili na wanawake zao.

*"Nitumie nafasi hii hadhimu kuwasihi wanaume,msione haya kuja kutoa taarifa ya Ukatili pindi mkeo anapo kukatili nenda kituo cha Polisi Dawati la jinsia litakusikiliza na kutafuta suluhisho la tatizo hilo nakuwafanya muishi kwa Amani na Upendo."* alisema inspector

Pamoja na hayo mengi bado katika Jarida letu limetoa taarifa ya elimu ya lishe,ambapo hapo tunakumbushwa kuwa mlo bora kwa watoto wetu itasaidia kuondokana na Udumavu ambao kwasasa kwa Halmashauri yetu ya Ludewa  tunataka kuutokomeza kabisa Udumavu.

Katika hatua nyingine hivi karibuni Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Sunday Deogratias alitangaza ajira 8 na mwisho wa kutuma barua za maombi ya kazi ni tarehe 08/06/2022 hivyo watanzania wote mnakumbushwa kutumia fursa hii kwa siku zilizo salia kuomba kazi.

Hali kadhalika wananchi wa Kata ya Milo Wilayani Ludewa wametoa hisia zao kwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuziinua kaya masikini kwa Kuziwezesha fedha ambayo imewafanya maisha yao yabadilike.

Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Mapogoro katani Milo wamesema TASAF imewawezesha na kufikisha kujiinua kiuchumi hukubwengi wao fedha hiyo wakiielekeza kwenye Mashamba na wengine wamenunua mifugo na kuifuga na kukarabati nyumba zao.

Lakini pia Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Sunday Deogratias ametuma salamu za pongezi kwa Kata ya Madilu kwa kuonesha ukomovu na shauku kubwa ya maendeleo ya Wilaya haswa katika eneo la elimu kwa kufanikiwa kujenga nyumba ya mwalimu wa shule ya msingi Madilu ambapo ujenzi wake unatarajia kukamilika mwaka huu.

Habari kubwa katika Jarida letu la leo Juni 03, 2022

 

Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Andrea Tsere anaendelea kuwaasa baadhi ya watu watakao dhubutu kukwamisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022.

Kauli hiyo anaitoa kila mahala anapo endelea na ziara yake ya Kuhamasisha na kuelimisha watanzania wote waliopo ndani ya Wilaya ya Ludewa huku akiwaeleza umuhimu wa Sensa ya kwa maendeleo ya taifa letu.

Aidha Mhe. Andrea Tsere alisesema "zoezi la Sensa ya Watu na Makazi kwa mwaka huu ni muhimu kwenye taifa letu, kwani kila mmoja wetu akihesabiwa serikali itajua namna ya kuhudumia wananchi wake haswa wakati wa kuandaa bajeti ukilinganisha na idadi ya Watu wake"

Kwa kuto hesabiwa mmoja utaifanya serikali ipate takwimu tofauti hivyo watu wangu kwanu wananchi wote tarehe 23/08/2022 kila mmoja anawajibu wa Kuhesabiwa asiwepo hata mmoja wa kukwepa jambo muhimu la kitaifa.


Donderdag, Junie 02, 2022

DC LUDEWA ATEMA NYONGO



Mkuu wa wilaya ya Ludewa Andrea Tsere  ametoa onyo kwa mtu yeyote atakayeonekana kuvuruga zoezi la Sensa ya watu na makazi na kuahidi kumchukulia hatua kali kwa mujibu wa sheria ya nchi ikiwemo kulipia faini kiasi cha fedha kisichopungua Ml.1, Jela miezi sita au vyote kwa pamoja.

Kauli hiyo ameitoa katika mikutano ya kutoa elimu juu ya zoezi hilo la Sensa ya watu na makazi iliyofanyika katika kata ya Luilo, Luhuhu pamoja na kata ya Manda.

Kwa mujibu wa Hakimu Mfawidhi wa Wilaya hiyo Isaac Ayengo amesema adhabu hizo zipo kwa mujibu wa sheria ya sensa kifungu namba 43(3) ambacho kinaeleza makosa ambayo raia hapaswi kuyafanya .

HABARI KUBWA KATIKA JARIDA LA LUDEWALEO JUNI 02, 2022

Habari kubwa katika Jarida letu la leo ni jengo la Ofisi kubwa ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wilaya ya Ludewa linalo jengwa katika Halmashauri hiyo huku ujenzi wake ukiendelea kwa kasi ukilinganisha na kipindi kilicho pita kwa sababu ya mvua kubwa zilizo kuwa zikiendelea kunyesha.

Kukamilika kwa jengo hilo litatatua kero ya ukosefu wa Ofisi za idara mbalimbali zilizotawanyika.

Lakini pia Ukamilikaji wa jengo hilo litakuwa ni jengo zuri ambalo litawavutia watu wengi kuja kulitembelea kutokana na uzuri wa jengo lenyewe na wengi watatamani kupiga picha katika eneo hilo.

Aidha katika jarida letu la leo habari kubwa iliyo gusa mioyo ya watu wengi ni kutoka pale Kata ya Luana ambapo, Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Ndg.Sunday Deogratias aliwaahidi wananchi wa Kata ya Luana  alipo kuwa akiwahutubia katika mkutano wa wawazi na kusema kuwa, Kata ya Luana ni miongoni mwa kata zinazo fanya vizuri haswa katika ukelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasà, Ujenzi wa vituo vya afya nk.

Hivyo kwa uunga mkono jitihada za wananchi wa Kata hii sasa nikiwa Kama Mkurugenzi nitatoa Bati 176 ambazo Mhe. Diwani Wilbard Mwinuka ameniomba.

Hivyo nawaombeni wananchi tuendelee kuiunga mkono serikali yetu kwa kuendelea kufanya kazi ili tutekeleze miradi yote inayo endelea kwenye kata hii "alisema Sunday Deogratias Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Ludewa" kauli hiyo aliitoa Mei 29, 2022.

Licha ya Miradi mingi inayo tekelezwa kwenye Wilaya ya ludewa, Diwani wa Kata ya Ludende  Mhe. Vasco Mgimba akishirikiana na wananchi wa Kata hiyo wamefanikiwa kuinua jengo la Mama na mtoto la kituo cha Afya cha  Ludende ambao Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ilitia mkono wake kuunga mkono juhudi za wananchi, lakini pia Diwani wa Kata hiyo bado amenyenyekea chini ya serikali kuomba kuungwa mkono ili kukamilisha jengo hilo ambapo awali serikali ilitupia mkono wake katika hengo hilo na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wilaya ya Ludewa bado amewapa Imani kubwa wananchi wa Kata hiyo kwa kusema kuwa,

Serikali inatambua mchango mkubwa wa wananchi wa Kata hiyo ndio maana Walipo omba Halmashauri isaidie kwa awamu ya kwanza ilitekeleza na kwasasa Mhe. Diwani kaomba tena na sisi Kama Halmashauri tutaaungana na wananchi kukamilisha jengo hilo kwa Bajeti ya Mwaka 2022/2023.

Katika hatua nyingine katika jarida letu la leo Juni 02, 2022 Sehemu ya juu inaelezea Ujenzi wa chuo cha Ufundi VETA kinacho jengwa Kata ya Lugarawa pale shaulimoyo, ujenzi wake unaendelea na kwasasa upo kwa asilimia 20% ambapo ukamilikaji wake ni  mwishoni mwa mwaka huu, na kusuasua kwa mradi huo ni kutokana na mvua kubwa zilizo nyesha kwa kipindi cha mwezi January hadi Aprili.

Pia neema nyingine yamwagika tangu kuumbwa kwa ulimwengi barabara ya kutoka Mbwila hadi Lifuma inaendelea na uchimbwaji ambapo kukamilika kwa barabara hiyo itakuwa imeokoa gharama kubwa za usafiri ukilinganisha na wakati huu wananchi hulazimika kusafiri kwa kutumia Ziwanyasa (Mitumbwi na Boti)

Jitihada za Mhe. mbunge wa Ludewa  Joseph Kamonga zinaendelea kuzaa matunda, na ikumbukwe kwamba Jana Mei moja aliweza kuhoji Bungeni mambo mbalimbali ikiwemo uendelezwaji wa nguvu

za wananchi wake.


 

Dinsdag, Mei 17, 2022



Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Waziri Waziri Kindamba jana Mei 12, 2022 alitembelea kiwanda cha muwekezaji mkubwa wa Parachichi Mjini Makambako katika mkoa wa Njombe kinachojulikana kwa jina la AvoAfrica.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa pamoja na mambo mengine alikagua shughuli mbalimbali zinazofanywa na muwekezaji wa kiwanda hicho haswa katika utaratibu mzima wa uchakataji wa Parachichi hadi hatua ya mwisho.

Katika hatua nyingine Mhe. Waziri Kindamba wakati akizungumza na wafanyakazi pamoja na wananchi wa maeneo hayo alisema kuwa;

Ndugu wananchi wa Mkoa wa Njombe na Watanzania wote, nitumie nafasi hii kuwahakikishia wawekezaji wote kuwa, Njombe ni sehemu salama ya uwekezaji na tunawakaribisha wawekezaji wote kuja kuwekeza katika Mkoa wa Njombe katika sekta ya Viwanda, Kilimo, Uvuvi, Utalii bila kusahau Madini kule Ludewa_ ,*

Aidha Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe Waziri Waziri Kindamba aliongeza kwa kusema kuwa;

Muwekezaji yeyote atakayekuja kuweka Mtaji wake Njombe tupo tayari kuwalinda kwa wivu mkubwa ili vijana wetu waendelee kupata Ajira.

Katika hatua nyingine Mhe. Mkuu wa Mkoa alisema kuwa Wawekezaji wanapokuja kuwekeza Njombe Serikali inapata faida kwa ulipwaji wa Kodi kutoka kwa wawekezaji hao lakini pia Wananchi wananufaika na mambo mbalimbali ikiwemo Ajira, mzunguko wa Biashara n.k.

Umuhimu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022

 

Umuhimu wa kipekee wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 ni pamoja na:-

  1. Kuisadia Serikali kupata taarifa za msingi zitakazosaidia mchakato wa utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025, mageuzi ya masuala ya afya na jamii, pamoja na ufuatiliaji wa ajenda za maendeleo za kimataifa;

  2. Taarifa za idadi ya watu husaidia katika mamlaka za wilaya katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo ambayo huakisi matakwa ya watu katika ngazi husika na kusaidia kwenye uwiano wa mgawanyo wa rasilimali;

  3. Taarifa za msingi za hali ya kidemografia, kijamii na kiuchumi za idadi ya watu na makazi za mipango katika ngazi zote;

  4. Kigawio katika kukokotoa viashiria vingine mfano Pato la mtu mmoja mmoja, Pato la Taifa, Ajira na ukosefu wa Ajira na kiwango cha uandikishaji wa wanafunzi;

  5. Taarifa itakayowezesha serikali kujua ongezeko la idadi ya watu, kwa mgawanyo na viashiria vingine, ambavyo ni muhimu kwa usimamizi wa mazingira; na

  6. Msingi wa utawala bora na ujumuishaji wa demokrasia. Takwimu sahihi za Sensa zinahitajika kwa ajili ya ugawaji wa majimbo ya uchaguzi kwa ufanisi, kurekebisha mipaka ya kiutawala katika serikali za mitaa.


Saterdag, Desember 14, 2019

CHUO TOKA NJOMBE CHAWANASUA VIJANA KWENYE JANGA LA ELIMU YA JUU NAFASI ZA MASOMO HIZI HAPA USIHANGAIKE KUANZIA DARASA LA SABA NAKUENDELEA MNAPOKELEWA

Kama utahitaji ufafanuzi zaidi piga simu au tuma ujumbe mfupi wa maadishi 0753121916 au  0620669137 utapewa ufafanuzi zaidi.

Wanafunzi wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Eckros Njombe Tanzania.
Hapa ni wanafunzi wakiwa na mkurugenzi wa chuo pamoja na walimu.

Vrydag, November 22, 2019

Mambo yatakayokuepusha na ugonjwa wa kisukari



Ugonjwa wa kisukari ni moja ya magonjwa yasiyoambukiza, ambayo husababishwa baada ya kongosho kushindwa kutengeneza 'insulin' ya kutosha ndani ya mwili.

Hukumu Ya Rais wa zamani wa TFF Jamal Malinzi na wenzake Kusomwa Disemba 5 Mwaka Huu



Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema itatoa hukumu dhidi ya Rais wa zamani wa TFF Jamal Malinzi na wenzake watatu December 05 mwaka huu.

Malinzi, Mwesigwa, Mwanga na Flora wanakabiliwa mashtaka 20 yakiwamo ya kula njama, kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na utakatishaji wa fedha Dola za Kimarekani 173,335.

Waziri wa Viwanda na Biashara Afanya Uteuzi wa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).




mubashara blog +255753121916