NAIBU
Waziri wa Elimu ,Sayansi na Teknolojia,William OleNasha,amefafanua
utaratibu wa kupata cheti mbadala/uthibitisho kwa mtu aliyepoteza cheti
ambapo ameeleza kuwa Baraza la Mitihani litafanya kazi hiyo kwa muda
usiozidi siku 30.
Ole
Nasha aliyasema hayo jana bungeni mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali
la Mbunge wa Mafinga Mjini,Cosato Chumi (CCM) lililokuwa likihoji ‘’Je
ni utaratibu gani unaotumika pale mtu anapopoteza cheti ili aweze kupata
cheti kingine’’?,Je ni unapata cheti halisi au nakala? na ni taratibu
gani anatakiwa kuzifuata mtu ili ombi lake lifanyiwe kazi ipasavyo na
bila kucheleweshwa?.