Dinsdag, Februarie 06, 2018

Dogo Janja ampa somo Edu Boy

'Hitmaker' wa Ngarenaro, Dogo Janja amemchana msanii Edu Boy kwa aina yake ya uimbaji ya kuwa-diss wasanii wenzake katika mashairi yake na kudai kuwa anachokifanya ni utoto mtupu na kwamba hawezi kufaidika na lolote.

Mbele ya kamera za eNEWZ Dogo Janja amesema kwamba msanii anapaswa kuimba kitu ambacho hata kizazi kijacho kikipata fursa ya kuskiliza nyimbo zao kitajifunza kitu kupitia mashairi ya msanii husika.

Dogo Janja ameendelea kusema kwamba "mpaka sasa tunasikiliza nyimbo walizoimba wasanii wa zamani kama kina Mbaraka Mwinshehe kwa kuwa waliimba nyimbo zenye maadili na zenye ujumbe kwa jamii lakini pale unapoamka na kuanza kuandika mashairi ya kumchana msanii mwenzio huwezi kuwa na historia nzuri kwenye sanaa".

Msanii huyo amedai kwamba Edu Boy ni kama mdogo wake kwenye sanaa kwa kuwa amemkuta kwenye sanaa na kusema kuandika wimbo unaowachana wasanii wezake inakuwa kama umeamka na mawazo yako alafu unaamua kuyamalizia kwa wasanii wezako kwani anachoamini ni kwamba hata ukiwachana wasanii wezako huwezi kufaidika kwa lolote.


Chrispiny kalinga blog

Chirwa ampita John Bocco kwa mabao

Mshambuliaji Obrey Chirwa wa Yanga amempita kwa mabao mahodha wa Simba John Bocco baada ya kufikisha mabao 10.

Serikali kutunga sheria ya kilimo ambayo itatoa mwongozo kwa wadau wa sekta ya kilim


Waziri wa kilimo Mh.Dkt.Charles Tizeba amesema serikali inakusudia kutunga sheria ya kilimo ambayo itatoa mwongozo na kanuni za kufuatwa na wadau wote wa sekta ya kilimo nchini ili kuongeza uwajibikaji zaidi na kuinua kilimo kwa shabaha ya kuondokana na kilimo cha mazoea

MSUKUMA AMWENDEA WAZIRI

Mbunge na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Joseph Msukuma amemshambulia kwa maneno Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina juu ya 'operation' anazozifanya za kionevu za kupambana na uvuvi haramu kwa kumwambia aache kufanya kazi kwa mihemuko.

CUF ya Maalim Seif yamshutumu Lipumba


Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma wa CUF kwa upande wa Maalim Seif, Mbarala Maharagande amefunguka na kuweka wazi kuwa Profesa Lipumba pamoja na genge lake wamepanga njama kuwafukuza madiwani wote wa CUF Dar es Salaam.

UN yafanya uteuzi katika kupambana na kutokomeza ukeketaji na ndoa za utotoni

February 6, 2018 ikiwa ni maadhimisho ya Siku ya Kupinga Ukeketaji duniani, Shirika la wanawake la Umoja wa Mataifa UN Women limefanya uteuzi.

Ahukumiwa kifo kwa shambulio Mogadishu

Mahakama ya kijeshi nchini Somalia, imemhukumu mtu mmoja adhabu ya kifo kwa kutekeleza shambulio mbaya zaidi nchini humo, mwezi Oktoba mwaka uliopita.

PETS KATA YA LUDEWA WAKAGUA MRADI WA MAJI UTAKAO WANUFAISHA WANANCHI WA KIJIJI CHA LUDEWA


 Meneja wa mamlaka ya maji Ludewa Bw.Mwinuka Gregory akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa Pets.

 siku kadhaa zimepita baada ya ukaguzi huo HABARI IMEANDIKWA NA 

Habari Ludewa Blog



WILAYANI LUDEWA WAMSINDIKIZA KWA MINOFU NA ZAWADI MKUU WA SHULE,,



MKUU WA SHULE ALIYE TUMBULIWA AAGWA KWA KEKI NA MINOFU MIZULI,,,


Brother, Joseph John Akiwaaga Watumishi wenzake,Wanafunzi pamoja na Wageni walioshiriki tukio hilo Jana,
Huyu ndie Mkuu mpya wa Shule ya Sekondari Montfort Brother, Masini

Waziri Mwigulu: “Mikoa ya Kaskazini inaongoza kwa wahamiaji haramu”


Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Mwigulu Nchemba amelitaka jeshi la polisi kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa na kwamba taasisi hiyo ndiyo inayoshughulika na haki za watu na wasipofanya kwa uadilifu yapo madhara makubwa kwa jamii na kutoka kwa wahalifu.

Bombardier Nyingine na Boeing 787 Kutua Nchini Julai Mwaka Huu


Ndege mbili; moja aina ya Bombardier na nyingine kubwa Boeing 787 yenye uwezo wa kubeba abiria 262 zilizonunuliwa na serikali, zinatarajiwa kuwasili nchini Julai mwaka huu.

Mahakama yaagiza Nabii Titto apime upya akili


MAHAKAMA ya Wilaya ya Dodoma imeagiza mkazi wa mtaa wa Ng’ong’ona Manispaa ya Dodoma Tito Machibya, maarufu kama ‘Nabii Tito’ (45) kupimwa akili upya katika Taasisi ya Afya ya Akili ya Mirembe Isanga mkoani Dodoma ili kujiridhisha kama ana matatizo ya akili.