Woensdag, Augustus 08, 2018

Walinzi Wauana kwa Risasi kisa deni la Sh. 30,000

Mlinzi  wa kampuni ya Lake Security, ameuawa kwa kupigwa risasi tumboni na mlinzi mwenzake baada ya kuzuka ugomvi kati yao wa kudaiana Sh. 30,000.

WCB yawapatia magari wasanii wake Lavalava na Mbosso

WCB yawanunulia magari wasanii wake, Mbosso na Lavalava hii ni mara baada ya Diamond Platnumz kuposti video clip kwenye Insta Story yake na kuonesha magari hayo hapo jana siku ya Jumanne.

NEC Yaijibu CHADEMA Kuhusu Uchaguzi Mdogo Jimbo La Buyungu




Hussein Makame-NEC
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Dkt. Athumani Kihamia amesema Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Buyungu ataendelea kutekeleza majukumu yake kwa kuwa malalamiko yaliyotolewa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ya kumkataa msimamizi huyo hayakufuata taratibu za kisheria.

Dinsdag, Augustus 07, 2018

Benki kuwakopesha wavuvi zana



BENKI ya Wananchi Tandahimba (Tacoba) mkoani Mtwara, imesema inatarajia kuwakopesha wavuvi ili kuongeza mtaji na kuboresha shughuli zao na hatimaye kuchangia pato la taifa.

Tetemeko la ardhi latokea Rukwa na Congo

 

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa  kipimo cha ritcher 4.4 na kina cha Kilomita 10 limetokea katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Rukwa na maeneo ya jirani usiku wa kuamkia leo Agosti 7, 2018

Kairuki Atema cheche kwa maofisa madini

 


WAZIRI wa Madini, Angellah Kairuki, amesema hatosita kumtumbua mara moja ofisa wa tume ya madini na ofisa migodi atakayethibitika kumiliki hisa kwenye kampuni za madini au kuwa na leseni ya kuchimba madini.

Watoto Wawili Wafariki Dunia Baada ya Nyumba Kuwaka Moto


Watoto wawili wa kike, mmoja wa mika miwili na mwingine wa miezi 6  wamefariki  dunia baada ya nyumba walimokuwa wamelala kuungua moto. Ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia leo Agosti 7 katika katika kijiji cha Rwazi kata ya Kikuku, Kagera.

Mkuu wa Mkoa Ataka Wahamiaji Haramu Wakamatwe Haraka na Kufungwa

Mkuu wa mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga ameiagiza Idara ya Uhamiaji kuanza msako wa kuwakamata wahamiaji haramu waliojificha kwenye mashamba na majumbani.

Matapeli 13 wa ile pesa Itume kwa Namba Hii wafikishwa Mahakamani


Watu 13 wamefikishwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi ikiwemo utakatishaji fedha wa Shilingi Milioni 154.

Wanachama wa CCM Monduli waandamana kumkataa Mbunge aliyetoka CHADEMA ( Julius Kalanga)


Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Monduli wameandamana kwenye ofisi za chama hicho wakitaka aliyekuwa Mbunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA), Julius Kalanga aliyejiunga na chama hicho kufuata utaratibu ikiwemo hatua za uteuzi wa nafasi ya kugombania ubunge.

Maandag, Augustus 06, 2018

Nanenane ya kisasa


WAZIRI wa Kilimo, Dk. Charles Tizeba amewataka waandaaji wa maonyesho ya kilimo na sherehe za wakulima Nanenane kuhakikisha kuanzia mwaka 2019 wanayaandaa katika sura mpya itakayoleta mabadiliko chanya kwa wakulima, wafugaji na wavuvi ili waweze kuzalisha kwa tija.

Mbao na mitego ya wanyama pori vya kamatwa Lindi


Na.Ahmad Mmow,Lindi.

MBAO 75  na mitego miwili  iliyokuwa inatumiwa na majangiri kutegea wanyama pori,kitongoji cha Namapwiya,Kijiji cha Mnyangala, Kata na karafa ya Mipingo,wilaya na mkoa wa Lindi,

Walimu watakiwa kufuata masharti na miongozo iliyowekwa na Serikali


Na. Thabit Madai, Zanzibar.

Walimu wa Skuli binafsi wametakiwa kuhakikisha wanafuata Masharti na miongozo iliyowekwa na serikali  ili kuimarisha  Elimu ya msingi na sekondari na kuongeza kiwango cha ufaulu nchini.