Woensdag, Mei 09, 2018

Tanzania yafungua ubalozi wake Israel, Mahiga aomba Israel ifungue ubalozi Dar es Salaam

Dkt Mahiga akikata utepe kuashiria ufunguzi wa ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel jijini Tel AvivHaki miliki ya pichaFOREIGN TANZANIA
Image captionDkt Mahiga akikata utepe kuashiria ufunguzi wa ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Israel jijini Tel Aviv
Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania Dkt. Augustine Mahiga amezindua rasmi ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Israel na kuitaka Israel nayo iharakishe kufungua ofisi ya ubalozi nchini Tanzania.

Al-Shabab wampiga hadi kifo mwanamke aliyedaiwa kuolewa mara 11 Somalia

Wanamgambo wa kiislamu wanadhibiti maeneo kadhaa nchini SomaliaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionWanamgambo wa kiislamu wanadhibiti maeneo kadhaa nchini Somalia
Mwanamke mmoja amepigwa na mawe mpaka kifo nchini Somalia baada ya mahakama moja inayoendeshwa na kundi la wanamgambo wa kiislamu, al-Shabab kumkuta na hatia ya kuolewa na wanaume wengi.

Ebola: Kenya yachukua hatua baada ya watu wawili kuthibitishwa kuwa na Ebola DR Congo

Mlipuko wa mwisho wa Ebola DR Congo ulikuwa 2017 ambapo watu 4 walifarikiHaki miliki ya pichaAFP
Image captionMlipuko wa mwisho wa Ebola DR Congo ulikuwa 2017 ambapo watu 4 walifariki
Serikali ya Kenya imeimarisha doria katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Jomo Kenyatta na vituo vingine vya mpakani baada ya visa vya ugonjwa wa Ebola kuripotiwa kaskazini magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Shamsa Ford Amjia Juu Harmonize Kwa Kuingilia Ndoa Yake

Msanii wa Bongo fleva kutoka label ya WCB Harmonize amepokea makavu live kutoka kwa mwanadada anayefanya vizuri kwenye tasnia ya Bongo movie Shamsa Ford baada ya kumuorodhesha mumewe Chidi Mapenzi Kwenye orodha ya Wolper.

Uingereza, Ufaransa, Ujerumani Zasikitishwa Na Maamuzi ya Trump Kujiondoa Mkataba wa Nyuklia wa Iran

Hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani, ya kutangaza kwamba nchi hiyo inajiondoa kwenye mkataba wa kimataifa wa mpango wa kuizuia Iran kutengeneza silaha za nuklia, JCPOA, imepokelewa kwa hisia kinzani na wabunge wa Marekani na viongozi mbalimbali ulimwenguni kote.

TMA yatabiri ujio wa mvua kubwa kwa siku tano

Mvua kubwa yatarajiwa kunyesha katika mikoa ya Dar es salaam, Tanga, Pwani na Visiwa vya Unguja na Pemba.

Mwanasayansi wa Australia kuuliwa na sindano ya sumu kesho

Mwanasayansi aliyesafiri kutoka Australia mpaka Uswiss David Goodall,  kwa ajili ya kuukatisha uhai wake kesho inatarajiwa kuwa ndiyo siku ya kuhitimisha maisha yake ya duniani baada ya madaktari kuchomeka sindano ya sumu katika mshipa.

TANZANIA YATIKISA ULIMWENGU KWA KUGUNDUA DAWA YA UKIMWI

Serikali imesema tayari nchi imeanza rasmi majaribio ya dawa kinga mpya inayozuia maambukizi ya virusi vya Ukimwi (PrEP), huku ikikanusha kuwapo kwa dawa inayotibu ugonjwa huo.

Sondag, Mei 06, 2018

Visa vya uhalifu wa kingono vyapitukia India

India rape arrest

Polisi upande wa Mashariki mwa India katika jimbo la Jharkhand wamearifu kuwa wamemkamata mtuhumiwa mkuu anayehusishwa na unyanyasaji wa kingono na mauaji ya binti mdogo .

Msikiti washambuliwa Afghanistan wakati wa swala

Afghanistan attack
Maafisa kutoka Mashariki mwa Afghanistan wanaarifu kuwa watu kumi na nne wamekufa na wengine na kadhaa walijeruhiwa katika mlipuko kwenye msikiti katika jimbo la Khost.

Watu sita wahofiwa kufa maji kisiwani Mafia

Mafia ,Tanzania

Haki miliki ya picha
Watu sita wanahofiwa kufa maji baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kupinduka bahari, karibu na Kisiwa cha Mafia Tanzania,kutokana na dhoruba kali.Mbunge wa jimbo la Mafia, mkoani Pwani Mbaraka Dau amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

RAIS MAGUFULI ATEMA CHECHE KWA VIONGOZI


Rais Dkt. John Magufuli amewataka viongozi wa serikali kuacha kutoza ushuru kwa wananchi wanaosafirisha bidhaa na mazao ambayo hayajafika uzito wa tani moja,  kwakuwa bunge mwaka 2017 lilipitisha sheria ya kufuta tozo zaidi ya 87 katika sekta ya kilimo.

Kitila Mkumbo atii agizo la Rais Magufuli

Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof. Kitila Mkumbo, ametekeleza kwa vitendo agizo alilopewa na Rais Magufuli, la kwenda kijijini Tundu, Wilayani Mikumi kushughulikia kero ya mradi wa maji kijijini hapo.