Woensdag, Mei 09, 2018

Al-Shabab wampiga hadi kifo mwanamke aliyedaiwa kuolewa mara 11 Somalia

Wanamgambo wa kiislamu wanadhibiti maeneo kadhaa nchini SomaliaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionWanamgambo wa kiislamu wanadhibiti maeneo kadhaa nchini Somalia
Mwanamke mmoja amepigwa na mawe mpaka kifo nchini Somalia baada ya mahakama moja inayoendeshwa na kundi la wanamgambo wa kiislamu, al-Shabab kumkuta na hatia ya kuolewa na wanaume wengi.

Shukri Abdullahi Warsame alishutumiwa kuolewa mara 11 bila kutalikiwa na waume zake waliopita.
Sehemu ya kiwiliwili chake kilifukiwa ardhini kichwa kikiachwa juu kisha akapigwa mawe na wanamgambo mjini Sablale mpaka umauti.
Mwaka 2014,wapiganaji wa al-Shabab walimpiga mwanamke mmoja na mawe baada ya kumshutumu kuolewa na wanaume wanne kwa siri, wilaya ya Barawe nchini humo.

mubashara blog +255753121916

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking