Sondag, Mei 13, 2018

ASKOFU WA ROMANI KATHORIKI NJOMBE ANENA MAZITO

Image result for bishop alfred maluma

Njombe

Na chrispin kalinga.

Kanisa la Romani Kathoriki Wilayani Njombe Mkoani Njombe leo katika ibada ya Misa ya pili  iliyo ongozwa na Askofu wa kanisa hilo baba Askofu ALFRED MALUMA ambayo ililenga haswa kuazimisha siku ya sikukukuu ya kupaa kwa Bwana Yesu Kristo ambapo amefundisha mambo mengi haswa kuwa heshimu wakina mama.


Akiyazungumza hayo Kanisani mbele ya wahumini kuwa watu wote wanatakiwa kuishi maisha matakatifu kipindi hiki cha nyakati za uzima huku akiwataka kumkumbuka bikira maria ambaye pia ndiye mama yake 
Yesu.
Askofu huyo amewapa kauli mbiu isemayo ‘Mama Maria huku wengine wakihitikia kwa kusema wetu sote’.

Sambamba na hayo kiongozi huyo amesema kuwa wote watubu Dhambi zao na kumfuata Bwana Yesu ili siku ya hukumu ikifika wawe wamekombolewa na akaongeza kwa kuwataka waumini wote kuwaheshimu wazazi wote haswa wakina mama.

Katika hatua nyingine Askofu huyo akawapokea wanachama wapya wa chama cha wawata {WWT} ambacho chama hicho ni chama cha umoja wa kinamama wa kathoriki Tanzania na akawapongeza kwa kujiunga katika chama hicho akawasihi wazidi kuomba mungu huku na kuwaombea wengine.

Kwa upande wao wakinamama wa kanisa hili wamezungumza na waandishi wa habari kuwa siku hii ya sikukukuu ya kupaa kwa Bwana Yesu kwa upande wao wameipokea vizuri kwa kumwomba mungu katika sara na pia wamebarikiwa kwa sikukukuu ya kuadhimisha miaka 150 ya kanisa kathoriki tangu lianzishwe kwake.


Pia Askofu akamaliza kwa kusema kuwa wote waishi maisha ya kumwomba Mungu na wazidi kuombiana kwa mungu ili kifanikisha safari ya kuelekea Mbinguni.


mubashara blog +255753121916

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking