Vrydag, Mei 11, 2018

Profesa Jay amtabiria Sugu kuwa Rais wa Tanzania

Mbunge wa Mikumi (Chadema), Joseph Haule ‘Profesa J’ amempongeza mbunge mwenzake wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ kwa kuhitimisha mafunzo ya kisiasa na kusema sasa Sugu, anasubiri kuwa Rais wa Tanzania.

Profesa J ametoa utabiri huo leo Mei 11, 2018 bungeni kabla ya kuanza kuchangia kwa bajeti ya wizara ya viwanda, biashara na uwekezaji ya 2018/19, ameanza kwa kusema;

“Natoa pongezi kubwa sana kwa pacha wangu aka Sugu kwa kuhitimu mafunzo huko ndani ambayo yameongeza ujasiri na CV yake ya kisiasa na natumaini sasa hivi hatakuwa rais wa Mbeya bali anakwenda katika mchakato wa kuwa Rais wa Tanzania huko mbeleni.”

Pongezi kama hizo, zimetolewa pia na mbunge wa viti maalum (Chadema), Devotha Minja ambaye amesema kilichompata Sugu ni harakati za ukombozi wa taifa hili.

Profesa J akichangia bajeti hiyo ya viwanda amesema mkoa wa Morogoro ulikuwa na viwanda vingi lakini vingi vimeshindwa kujiendesha na kushauri uchunguzi ufanyike, ili kuona wapi tumejikwaa

mubashara blog +255753121916

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking