Woensdag, Mei 09, 2018

TMA yatabiri ujio wa mvua kubwa kwa siku tano

Mvua kubwa yatarajiwa kunyesha katika mikoa ya Dar es salaam, Tanga, Pwani na Visiwa vya Unguja na Pemba.

Utabiri huo umetolewa na Mamlaka ya Utabiri wa Hali ya Hewa Nchini (TMA), ambao umeeleza kuwa kiwango hicho cha mvua kilitarajiwa kuanza jana usiku.

Kwa mujibu wa utabiri huo kiwango cha mvua hiyo kitaendelea kwa siku tano hasa wanaoishi mabondeni, wametakiwa kuchukua tahadhari.

TMA imeeleza kwamba athari zinazoweza kutokea ni mafuriko ambayo yatasababisha msongamano wa magari na watu hali itakayochelewesha usafiri na usafishwaji maeneno ya mjini.

Aidha kwa siku ya jana asubuhi kulikuwa na wingu zito lililoashirijia ujio wa mvua kubwa, lakini haikunyesha mvua hiyo kama ilivyotarajiwa huku asubuhi ya leo majira ya saa kumi na mbili asubuhi katika baadhi ya maeneo jijini Dar es salaam imenyesha mvua ambayo imedumu kwa kipindi kifupi.
mubashara blog +255753121916

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking