Maandag, Augustus 06, 2018

Wawili Wafariki Dunia kwa Kufukiwa na Kifusi

Watu wawili wamefariki dunia kwa kufukiwa na kifusi cha udongo wakati wakichimba madini ya dhahabu katika machimbo madogo yaliyoko mtaa wa Buguti Kata ya Turwa wilayani Tarime.


Akizungumza leo Jumatatu Agosti 6, 2018 Kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Tarime/Rorya, Henry Mwaibambe amesema tukio hilo limetokea jana Jumapili Agosti 5 na  kuwataja waliofariki kuwa ni Bisaku Chacha (19) na Charles Mairo (18).

Amesema marehemu waliingia kwenye shimo lililokuwa limeachwa kwa siku nyingi wakitafuta mawe ya dhahabu matokeo yake waliangukiwa na mawe hayo.

Mzazi wa Charles, Mairo Wembe amesema hakuziamini taarifa za mwanae kufariki dunia, baada ya kurejea nyumbani ndio aliamini.



mubashara blog +255753121916

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking