Woensdag, Februarie 28, 2018

Nigeria: Raia 1,130 wakombolewa

Takriban raia 1,130 wamekombolewa na washukiwa 37 wa kundi la wanamgambo wa Boko Haram,wameuwa katika mashambulizi yaliyotekelezwa kwa pamoja na vikosi vya majeshi ya Cameroon na Nigeria,kuzunguka jimbo la ziwa Chad.

Taarifa iliyotolewa na msemaji wa jeshi la Nigeria,kanali Onyema Nwackukwu,operesheni hiyo imefanyika katika mpaka wa vijiji vya Kusha-Kucha, Surdewala, Alkanerik, Magdewerne na Mayen na kuharibu kambi kadhaa za Boko Haram,na kukamata silaha,zikiwemo bunduki nyingi aina ya mashine gun na bunduki za kutungulia ndege.

Kanali Nwackukwu,amesema,raia 603 walikombolewa katika ameneo ya Kusha-Kucha, Surdewala, Alkanerik, Magdewerne na vijiji vya Mayen

Chrispiny kalinga blog

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking