Saterdag, Februarie 03, 2018

Tume yaundwa kufuatilia korosho zenye kokoto


Serikali mkoani Lindi imeunda timu ya kuchunguza matukio ya baadhi ya wakulima kuchanganya mchanga na korosho kwa nia ya kuongeza uzito wakati wa kupima kwenye mizani,
ili hatua za kisheria zichukuliwe kwa watakaobainika kufanya hhujuma hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bw. Godfrey Zambi amewaambia waandishi wa habari mjini Lindi kuwa, korosho iliyochanganywa na mchanga kugundulika kwenye ghala la Buko mjini humo na korosho nyingine iliyochanganywa na kokoto za lami iligundulika nchini Vietnam baada ya kusafirishwa kutoka Tanzania, ambapo mwenye korosho hizo alidai alizinunua wilayani Liwale mkoani humo.

Amesema baada ya kupata taarifa hizo zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na kuchafua taswira ya Tanzania kibiashara, imemlazimu kukutana na viongozi wa mkoa kujadili suala hilo na hatimaye kuunda timu ya uchunguzi wa matukio hayo ili hatua zichukuliwe haraka.

Pamoja na uchunguzi unaoendelea, Mkuu huyo wa Mkoa ameeleza kuwa baadhi ya viongozi wa Chama cha Ushirika cha Pangatena wilayani Lindi wanashikiliwa kwa uchunguzi na kusimamishwa kwa bodi ya chama hicho baada ya kubainika korosho walizofikisha kwenye ghala kuu la BUCCO zina viroba vya mchanganyiko wa korosho na mchangaTume

Chrispiny kalinga blog

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking