Saterdag, Maart 10, 2018

Dogo Janja akoshwa na mwanamke huyu

KATIKA kuisindikiza Siku ya Wanawake Duniani, iliyofanyika juzi (Alhamisi), mkali wa michano Bongo, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’, amefunguka kwamba, kwa upande wake mwanamke ambaye amemkosha kwa mwaka huu ni mjasiriamali, Carol Ndosi.

Akipiga stori na Mikito Nusu Nusu, Dogo Janja alisema, Carol amemvutia kutokana na namna anavyojituma hata kuiingizia serikali pato la taifa.

“Carol kiukweli ‘ananiinsipaya’ sana. Ni mwanamke shujaa kwangu kwa mwaka huu. Tazama matamasha yake aliyokuwa anaandaa kama vile la Nyama Choma Festival. Unaona kabisa ni mbunifu na kupitia matamasha hayo ameweza kuliingizia taifa pato kubwa!” Alimaliza Dogo Janja

mubashara blog +255753121916

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking