Donderdag, Maart 15, 2018

Kina Pogba na Lukaku kuiponza Man United

London, England. Kuna wasiwasi Manchester United kwamba siku moja Glazer family watauliza wapi fedha zao zinapotumika.


Miaka mitano kabla ya Sir Alex Ferguson hajastaafu alitumia pauni 71milioni kununua wachezaji katika kipindi hicho alifanikiwa kutwaa mataji matatu Kombe la Ligi na kufanikiwa kufuzu fainali mbili za Ligi ya Mabingwa.

Lakini miaka mitano baada ya kuondoka, ametumia pauni 490milioni na mafanikio yake yakiwa ni Kombe la FA, Kombe la Ligi na Europa Ligi.

Hata hivyo hali hiyo inakuja baada ya timu hiyo kushindwa kuingia katika robo fainali ya Lihi ya Mabingwa.

Kuna sababu nyuma ya kuongezeka kwa dau hilo, kama kuongezeka kwa ada za uhamisho tofauti na ilivyokuwa kwa kikosi cha Sir Alex.

Lakini nyuma ya hilo kunaweza kumfanya Glazers kuuliza kuwa fedha haiwezi kununu mafanikio au ni jinsi fedha hizo zinavyotumika.

"Kila kitu kimebadilika," alisema Jose Mourinho Jumanne usiku wakati alivyoulizwa jinsi gani Man United itarudisha heshima yake Ulaya.

Tatizo kumebadilika kila kitu katika miaka hii mitano ndani ya Man United kuanzia makocha, wachezaji, lakini wameshindwa kushindana na Chelsea, Leicester au Manchester City katika kuwania mbio za ubingwa wa Ligi Kuu England hachana na kushindana na miamba mingine Ulaya.

mubashara blog +255753121916

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking