Sondag, Februarie 04, 2018

Lulu Diva apokonywa kila kitu na Mpenziwe?

 
IMEVUJA! Ukiachana na habari ya kudaiwa kupangishiwa nyumba na kununuliwa gari mpya aina ya Jeep na kigogo, imebainika kuwa msanii huyo amepokonywa kila kitu
alichokuwa amepewa na mpenzi wake wa zamani aitwaye Joho.

Hivi karibuni, Lulu Diva aliripotiwa kuwa amepangiwa nyumba na kupewa gari jipya ambapo aliibuka sosi mwingine na kudai kuwa Lulu si mkweli, aliyenunua gari hilo ni mpenzi wake Joho ambaye alikuwa akiishi naye kinyumba kwa takriban miaka mitatu kiasi cha kufikia hatua ya kutolewa mahari ambayo ilirudishwa hivi karibuni na hata hivyo gari hilo amepokonywa hayuko nalo tena.

Akipiga stori na Risasi Jumamosi kwa sharti la kutotajwa jina sosi huyo alisema kuwa anawajua vilivyo Lulu na Joho kwa sababu Joho ni rafiki yake hivyo anachokisema yeye ana uhakika nacho kwamba Lulu hajanunuliwa gari bali ni lile lile alilopewa na Joho.

“Hivi mnajua kuwa huyo Lulu ni muongo mbona gari analosema amepewa na kigogo ni la rafiki yangu Joho alimnunulia na walikuwa wakiishi pamoja ila kwa sasa ameachana naye na ninavyojua amechukua vitu vyake.

“Hii yote ilikuja baada ya jamaa kumshtukia kuwa Lulu anatembea na msanii mwenzake, Rich Mavoko,” alisema sosi huyo.


Chrispiny kalinga blog

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking