Saterdag, Februarie 03, 2018

Magufuli awatunuku 197


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewatunuku kamisheni maofisa wanafunzi 197 wa Jeshi la
Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Sherehe hizo zimefanyika leo Februari 3, 2018 katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam, ambapo maofisa hao wapya ni wa Tanzania na kutoka nchi marafiki,  waliopata mafunzo katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli mkoani Arusha.

Katia tukio hilo ambalo lilipambwa na magwaride kutoka kwa Wanajeshi hao, lilihudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Kitaifa.

Miongoni mwa waliotunukiwa kamisheni hizo wanawake ni 28, na waliobaki ni wanaume.

Chrispiny kalinga blog

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking