Saterdag, Februarie 03, 2018

Rais Trump awasiliana na viongozi wa Japan na Korea Kusini


Rais wa Marekani Donald Trump amewapigia simu viongozi wa Japan na Korea Kusini siku chache kabla ya michezo ya Olimpiki
kuanza nchini Korea Kusini.

Kwa mujibu wa habari,Trump amefanya mazungumzo na waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe.

Viongozi hao wawili wamezungumzia mfumo wa ulinzi wa makombora wa Japan na vilevile uhamisho wa ngome ya Marekani katika kisiwa cha Okinawa.

Japan na Korea Kusini zimekuwa zikijitahidi kuidhibiti Korea Kaskazini kutofanya majaribio ya makombora ya nyuklia.

Korea Kaskazini ilirusha kombora la nyuklia mnamo mwezi Novemba mwaka jana.


Chrispiny kalinga blog

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking