Saterdag, Februarie 03, 2018

Uchimbaji mafuta ya Petroli mkoani Morogoro kuanza Septemba 2018

Serikali imesema mradi wa uchimbaji mafuta katika Kisima kilichoanishwa kuchimbwa kwenye eneo la kijiji cha Ipera Asilia, kwenye hifadhi tengefu ya bonde la Kilombero, mkoani Morogoro, unatarajiwa kuanza rasmi mwezi Septemba, 2018 ambapo kisima hicho kinakadiriwa kuwa na mafuta kuanzia lita milioni 180 hadi 200.

Akizungumza jana Februari 2, 2018 katika kipindi cha maswali na majibu kwenye kikao cha nne cha mkutano wa 10 wa Bunge mjini Dodoma, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amesema kinachosubiriwa ni kibali kutoka Baraza la Mazingira nchini (NEMC) na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), ili uchimbaji huo uanze rasmi.

“Mkataba ulishasainiwa tangu mwaka 2012 kilihobaki ni utekelezaji wa uchimbaji na ugunduzi wa mafuta, mafuta yanayotarajiwa kuchimbwa kwenye eneo hilo yanafikia milionii 180 hadi 200, mtaji ni mkubwa na utakua na manufaa kwa wananchi wako na nchi kwa ujumla,” alisema na kuongeza.

“Kinachosubiriwa ni kibali cha mazingira kutoka NEMC na mamlaka ya TAWA, mwezi Julai mwaka huu tumehakikishiwa mkataba utapatikana na Septemba uchimbaji utaanza rasmi.”

Serikali kupitia shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) liliingia mkataba wa utafiti na uchimbaji wa gesi na uvunaji mafuta na Kampuni ya Mafuta na gesi ya Swala (Swala Oil), ambapo katika utekelezaji wa mkataba huo iligundulika kuwepo kwa wingi mafuta ya petrol na gesi katika vijiji vya Mtimbira

Chrispiny kalinga blog

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking