Maandag, Februarie 05, 2018

Kufuatia kifo cha Kingunge, CCM yasitisha kampeni kushiriki mazishi



Uongozi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam umesitisha kampeni za nje kwa siku moja (leo) kwa ajili ya kushiriki mazishi ya mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru.


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Siasa na Uenezi wa chama hicho, Simon Mwakifwamba imeeleza kuwa wanachama, makada na viongozi watashiriki kikamilifu katika msiba huo, hivyo hakutakuwa na kampeni za nje.

Alisema watazingatia ratiba iliyotolewa na msimamizi wa msiba huo Omary Kimbau, hivyo wanaCCM wafike mapema kwa ajili ya kumpumzisha kwenye makazi ya milele komredi Kingunge.

Chrispiny kalinga blog

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking