Vrydag, Februarie 02, 2018

Mtoto wa Fidel Castro amejiua



Mtoto wa Mwana mapinduzi na Rais wa kwanza wa Cuba Fidel Castro, Fidel Ángel Castro Díaz-Balart, mwenye umri wa miaka 68 amejiua akiwa mji mkuu wa
Havana.

Amekutwa amefariki February 1, 2018 na inadaiwa alikuwa anatatizwa na msongo wa mawazo.

Castro Díaz-Balart alifahamika sana kama “Fidelito” na alikuwa mtoto wa kwanza wa rais huyo wa zamani wa Cuba aliyefariki dunia November 2016.

Alikuwa mshauri wa kisayansi wa Baraza la Serikali ya Cuba na alihudumu kama makamu rais wa Chuo cha Sayansi cha Cuba pia alifanya kazi kama Mwanafizikia ya nyuklia.

Gazeti rasmi la Serikali ya Cuba la Granma limeandika hivi>>> “Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa ametibiwa na kundi la madaktari kwa miezi kadha kutokana na msongo wa mawazo, alijitoa uhai asubuhi hii,”

Runinga ya taifa imesema amekuwa akipokea matibabu miezi ya karibuni kama mgonjwa wa kutibiwa na kurudi nyumbani, baada yake kulazwa hospitalini kwa muda.


Chrispiny kalinga blog

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking