Dinsdag, Februarie 06, 2018

Prof. Palamagamba Amesema Magufuli anamamla ya Zanzibar


Waziri wa katiba na sheria Profesa. Palamagamba Kabudi amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli ana mamlaka yote ya kutoa maagizo kwa Mawaziri ambao wapo ndani ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Waziri Kabudi ametoa ufafanuzi huo leo (Jumanne) katika mkutano wa 10 kikao cha sita cha Bunge kinachoendelea mjini Dodoma wakati alipokuwa akijibu swali la nyongeza kutoka kwa Mbunge Juma kombo Hamadi alipotaka kufahamu Rais Magufuli ana mamlaka gani kikatiba ya kutoa maagizo kwa Waziri aliyepo katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

"Rais wa Muungano wa Tanzania anayo mamlaka ya mambo yote yanayohusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama nchi huru", amesema Prof. Palamagamba.

Pamoja na hayo,  Prof. Palamagamba ameendelea kufafanua baadhi ya mambo kuwa "katika masuala yote yanayohusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mkuu wa nchi ni mmoja tu tena ambaye ni Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na yeye peke yake ndio Amri Jeshi. Hakuna mtu mwingine yeyote wa kuyaamuru majeshi ya Tanzania isipokuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sababu yeye ndio kiongozi mkuu wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania".

Kwa upande mwingine, Prof. Palamagamba amesema Rais wa Zanzibar ni wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar mwenye heshima na hadhi ya urais kwa mambo yote yasiyokuwa ya Muungano yanayohusu Zanzibar ambapo pia ni Mjumbe wa Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nafasi yake hiyo.

Chrispiny kalinga blog

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking