Woensdag, Februarie 07, 2018

Tetemeko la ardhi laangusha Maghorofa na kuua



Taarifa katika vyombo vya habari vya kimataifa leo February 7, 2018 ni kuhusiana na tukio lililotokea katika mji wa
Hualien nchi Taiwan ambapo majengo marefu yameporomoka na kusababisha vifo vya watu wawili na wengine zaidi ya 200 wakijeruhiwa huku 150 wakiwa wamepotea.
Majengo hayo yameporomoka baada ya kutokea kwa tetemeko la ardhi katika mji huo lenye kipimo cha 6.4 lililoupiga mji huo wa kitalii usiku wa kuamkia Jumatano ya leo.
Inaelezwa kuwa watu wengi waliokuwa ndani ya majengo hayo bado wamenasa humo na juhudi za kuwanasua zinaendelea. Mji huo unakadiriwa kuwa na wakazi takribani 100,000.
Chrispiny kalinga blog

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking