Woensdag, Januarie 31, 2018

Hii ndio gharama ya passport za kielektroniki

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt.  Mwigulu Nchemba amesema kuwa gharama mpya ya hati ya kusafiria ya kielektroniki itakuwa Sh. 150,000.

Dk Nchemba amesema hayo leo  wakati wa uzinduzi wa Hati ya kusafiria ya kielektroniki jijini Dar es Salaam ambapo imezinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Aidha Dkt. Miwgulu Nchemba amesema kuwa Pasipoti hizo zitakuwa na ukurasa zaidi ya mmoja  na mwonekano mpya.

“kiasi cha gharama hiyo  ni sawa na Sh15,000 kwa mwaka kwa sababu itatumika kwa miaka 10. Gharama za kupata pasipoti sasa ni TSh.50,000 na hutumika kwa miaka 10 tangu zilipotolewa,“ amesema Dkt. Mwigulu.

Hata hivyo Rais Magufuli amesema kuwa gharama ya laki moja na nusu bei hiyo ni ya juu kidogo kuliko bei ya sasa . huku kieleza kuwa bei hiyo imezingatia ubora wa utenngenezaji wa Pasipoti hiyo.


chrispiny kalinga

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking