Dinsdag, April 10, 2018

Mashindano ya kuwabeba wake yafanyika Uingereza

Mshindi wa mchuano wa kubeba mkeHaki miliki ya pichaPA
Image captionMshindi wa mchuano wa kubeba mke
Haya ni mashindano ya 11 ya mbio za kubebana nchini Uingereza.
Chris Hepworth, akiwa amembeba Tanisha Prince kutoka West Drayton, London, alikimbia na kuibuka mshindi wa mbio za umbali wa mita 380.

Waandaaji wa michuano hiyo wanasema zoezi hilo lilianza mwezi June mwaka 793 AD.
Michuano inahusisha umbali wa mita 380 zenye vikwazo kukiwa na miinuko na miteremkoHaki miliki ya pichaPA
Image captionMichuano inahusisha umbali wa mita 380 zenye vikwazo kukiwa na miinuko na miteremko
Washindani walikimbia umbali wa mita 15 kupandisha kwenye mwinuko na kushuka ambapo wameeleza kuwa ni kazi ngumu.
Washindani si lazima wawe na ndoa lakini angalau wawe marafiki.
Chris Hepworth, alimbeba Tanisha Prince, aliibuka mshindiHaki miliki ya pichaPA
Image captionChris Hepworth, alimbeba Tanisha Prince, aliibuka mshindi
Sheria inasema wenza wawe na zaidi ya miaka 18 na uzito wa kilo 50 na kuna adhabu ikiwa utamuangusha mwenza wako, ikiwa uzito ni chini ya kilo 50 aliyembeba analazimika kubeba furushi lenye vikopo ili kuongezea uzito.
Mshindi anasema kupanda mlima ilikuwa rahisi kuliko kuteremka.
Washindi wataenda kwenye michuano ya dunia mwezi Julai nchini Finland
Bwana Hepworth ana matumaini ya kushinda.
Watu takriban 50 walishirikiHaki miliki ya pichaPA
Image captionWatu takriban 50 walishiriki
Waandaaji walitoa tahadhari wakisema kuwa ''kumbeba mke kunaweza kuwa jambo la hatari, kunakoweza kusababisha majeraha kama ya uti wa mgongo, kuvunjika miguu na mikono, majeraha usoni, kwenye fuvu la kichwa na hata kifo."
Ben and Hannah Brackenbury waliingia kwenye michuano hiyo wakiadhimisha mwaka mmoja wa ndoa yaoHaki miliki ya pichaPA
Image captionBen and Hannah Brackenbury waliingia kwenye michuano hiyo wakiadhimisha mwaka mmoja wa ndoa yao
Ben na Hanna Brackenbury waliingia kwenye mashindano hayo kuadhimisha mwaka wa kwanza wa kumbukumbu ya ndoa yao
Wenza hao wamesema walikuwa wakifanya mazoezi kwenye bustani na kwenye mvua wakijiandaa na michuano.
Mitindo mbalimbali ya kubebana ilishuhudiwaHaki miliki ya pichaPA
Image captionMitindo mbalimbali ya kubebana ilishuhudiwa
Mshindi alipata pipa lenye bia anayeshika nafasi ya mwisho anapatiwa tambi na chakula cha Mbwa.
Washindi watakwenda kushiriki michuano ya dunia nchini FinlandHaki miliki ya pichaPA
Image captionWashindi watakwenda kushiriki michuano ya dunia nchini Finland
Aina hii ya ubebaji imeelezwa iliwafanya wakimbie kwa kasiHaki miliki ya pichaPA
Image captionAina hii ya ubebaji imeelezwa iliwafanya wakimbie kwa kasi
Michuano ya dunia itafanyika mwezi JulaiHaki miliki ya pichaPA
Image captionMichuano ya dunia itafanyika mwezi Julai

mubashara blog +255753121916

Geen opmerkings nie:

Plaas 'n opmerking